Mwanzo 50:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200211 Wakanana wenyeji wa inchi hiyo, walipoona maombolezo yaliyofanyika kwenye uwanja wa kupepetea ngano wa Atadi, wakasema: “Maombolezo haya ya Wamisri, kweli ni makubwa!” Kwa hiyo, pahali pale pakaitwa Abeli-Misri, napo pako ngambo ya muto Yordani. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Walipeleka vilevile sanamu za zahabu za panya kulingana na hesabu ya miji yote ya Wafilistini iliyotawaliwa na wakubwa watano wa Wafilistini. Miji hiyo ilikuwa yenye kuzungukwa na kuta na vijiji ambavyo havikuzungushiwa kuta. Lile jiwe kubwa kwenye shamba la Yoshua wa Beti-Semesi, pahali ambapo walilipeleka Sanduku la Yawe, ni ushuhuda wa tukio hilo mpaka leo.