Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 5:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Alikuwa akishirikiana na Mungu, akatoweka, kwa maana Mungu alimupeleka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 5:24
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini yeye akasema: ‘Yawe aliyeniongoza katika maisha yangu, atamutuma malaika wake aende pamoja nawe na kukufanikisha katika safari yako. Nawe utamutwalia mwana wangu muke kutoka kwa jamaa yangu na nyumba ya baba yangu.


akaendea wandugu zake, akawaambia: “Kijana hayuko, nami niende wapi?”


Baba yao Yakobo, akawaambia: “Munaniondolea watoto wangu! Yosefu hayuko, Simeoni hayuko, sasa munataka kumutwaa Benjamina. Hayo yote yanaanguka juu yangu!”


Enoki alikuwa anashirikiana na Mungu. Kisha kuzaa Metusela, Enoki aliishi miaka mia tatu, na kupata wana wengine na wabinti.


Enoki aliishi miaka mia tatu makumi sita na mitano.


Wakati Metusela alipokuwa na umri wa miaka mia moja makumi nane na saba, akazaa Lameki.


Hizi ndizo habari za Noa na uzao wake. Noa alikuwa mwenye haki na mukamilifu kati ya watu wa wakati ule. Aliishi katika ushirika na Mungu.


Wakati ulifika ambapo Yawe alitaka kumupandisha Elia mbinguni katika upepo wa kuzungukazunguka. Elia na Elisha walikuwa katika njia, wakitoka Gilgali.


Elia akajibu: “Ombi lako ni gumu. Hata hivyo, ikiwa utaniona wakati nitakapoondolewa kwako, itafanyika vile kwako. Lakini usiponiona, basi haitafanyika vile.”


Walipokuwa wanatembea na kuongea, kwa rafla gari la moto lililokokotwa na farasi wa moto likawatenganisha. Naye Elia akanyanyuliwa mbinguni katika upepo wa kuzungukazunguka.


Elisha alipoona tukio hilo, akalia: “Baba yangu, baba yangu! Ulikuwa wa lazima kuliko magari ya Israeli na wapanda-farasi wake!” Basi, Elisha hakumwona tena Elia. Halafu Elisha akashika nguo zake na kuzipasua vipande viwili.


Wanaongozwa kama kondoo mpaka katika kuzimu; kifo ndiye muchungaji wao. Wanashuka moja kwa moja katika kaburi. Miili yao inaozea huko. Kuzimu inakuwa makao yao.


Wewe unaniongoza kwa mashauri yako; na kwa mwisho utanipokea kwenye utukufu.


Yawe anasema hivi: Sauti imesikilika katika muji wa Rama, maombolezo na kilio cha uchungu. Rakeli anawalilia watoto wake, wala hataki kufarijiwa kwa ajili yao, maana wote hawako tena.


“Sauti inasikilika toka Rama, kilio na malalamiko mengi. Ni Rakeli anayewalilia watoto wake, naye hataki kufarijiwa, kwa maana hawako tena.”


Yesu akamujibu: “Kweli ninakuambia wewe: leo hii utakuwa pamoja nami katika Paradizo.”


Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.


Ni Enoki, mutu wa kizazi cha saba tangu Adamu, ndiye aliyetabiri zamani juu yao, akisema: “Musikilize, Bwana atakuja pamoja na maelfu na maelfu ya wamalaika zake watakatifu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ