Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 5:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Enoki alikuwa anashirikiana na Mungu. Kisha kuzaa Metusela, Enoki aliishi miaka mia tatu, na kupata wana wengine na wabinti.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 5:22
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.


Lakini yeye akasema: ‘Yawe aliyeniongoza katika maisha yangu, atamutuma malaika wake aende pamoja nawe na kukufanikisha katika safari yako. Nawe utamutwalia mwana wangu muke kutoka kwa jamaa yangu na nyumba ya baba yangu.


Kisha Israeli akamubariki Yosefu, akisema: “Mungu ambaye babu zangu Abrahamu na Isaka walimutii katika maisha yao, Mungu ambaye ameniongoza katika maisha yangu mpaka leo,


Wakati Enoki alipokuwa na umri wa miaka makumi sita na mitano, akazaa Metusela.


Enoki aliishi miaka mia tatu makumi sita na mitano.


Alikuwa akishirikiana na Mungu, akatoweka, kwa maana Mungu alimupeleka.


Hizi ndizo habari za Noa na uzao wake. Noa alikuwa mwenye haki na mukamilifu kati ya watu wa wakati ule. Aliishi katika ushirika na Mungu.


Naye Yawe atatimiza ahadi yake aliyotoa aliponiambia kwamba, ikiwa wazao wangu watatii amri zake na kumutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wote, hakutakosekana mumoja wao kwa kutawala Israeli nyakati zote.


“Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote na kutenda mazuri mbele yako.” Hezekia akalia kwa uchungu sana.


Nitatembea mbele ya Yawe, katika inchi ya watu wenye kuwa wazima.


Wimbo wa safari za kidini. Heri wote wanaomwabudu Yawe, wanaoishi kufuatana na amri zake.


Siku zote Yawe ni mbele yangu; yeye yuko pamoja nami, wala sitatikisika.


Lakini mimi ninaishi katika ukamilifu; unihurumie na kunikomboa.


Ee Mungu, nitatimiza ahadi zangu kwako; nitakutolea sadaka za shukrani,


Unifundishe njia yako, ee Yawe, nipate kuwa mwaminifu kwako; uongoze moyo wangu nikuheshimu.


Halafu Yawe akamwambia Musa: “Mimi nitawanyeshea mikate kutoka mbinguni. Kila siku watu watatoka na kukusanya chakula cha siku hiyo. Kwa njia hii nitawapima nione kama watafuata sheria zangu au hawatazifuata.


Unipeleke, tuende haraka, mufalme amenileta katika chumba chake. Tutafurahi na kukushangilia pamoja, tutasifu mapenzi yako kuliko divai. Wabinti wana haki ya kukupenda!


Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.


Nitatembea kati yenu na kuwa Mungu wenu nanyi mutakuwa watu wangu.


Watu wawili wanaweza kusafiri pamoja bila kupatana kwanza?


Mataifa mengine yanafuata njia zao, kwa kuitegemea miungu yao, lakini sisi tunafuata njia zetu kwa kumutegemea Yawe, Mungu wetu, milele na milele.


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


Mafundisho yao yalikuwa ya kweli nao hawakufundisha uongo hata kidogo. Mimi na wao tulikaa kwa amani. Si kwamba walitenda haki tu, lakini waliwafundisha wengine kutotenda maovu.


Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


Wakati ule, kanisa lilikuwa na amani katika Yudea yote, Galilaya na Samaria. Vilevile lilizidi kupata nguvu na kuendelea kumwogopa Bwana, nalo liliongezeka kwa musaada wa Roho Mutakatifu.


Basi sasa hakuna azabu kwa wale wanaoungana na Yesu Kristo.


Kwa ngambo ingine, kila mutu aendelee kuishi kufuatana na zawadi aliyopewa na Bwana na kufuatana na vile alivyokuwa mbele ya kuitwa na Mungu. Hii ndiyo kanuni ninayofundisha katika makanisa yote.


Kuna ulinganisho gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu Mwenye Uzima kama vile yeye mwenyewe alivyosema: “Nitakaa na kuishi pamoja nao, nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”


Muangalie vizuri mwenendo wenu. Musiishi kama wajinga lakini muishi kama wenye hekima.


musisikilize maneno ya nabii huyo au mutabiri wa kutumia ndoto, kwa maana Yawe, Mungu wenu, anawatumia kwa kuwajaribu kusudi ajue kama munamupenda yeye Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.


“Yawe atawafanya kuwa watu wake watakatifu kama vile alivyowaahidi, kama mukitii amri zake yeye Yawe, Mungu wenu, na kufuata njia zake.


Mutafuata njia yote Yawe, Mungu wenu, aliyowaamuru kufuata kusudi mambo yenu yawaendekee vizuri na mupate kuishi muda murefu katika inchi mutakayotwaa ikuwe mali yenu.


Hivi, mutaweza kuishi sawa Bwana anavyotaka na kumupendeza katika mambo yote. Kwa njia hiyo mutafikia kufanya matendo mema ya kila namna na kuzidi kumujua Mungu.


Mukuwe na mwenendo wa hekima mbele ya watu wanaokuwa wa inje ya kanisa, mukitumia vema kila wakati munaoupata.


Sisi tuliwaonya, tuliwafariji na kuwasihi sana muishi sawa inavyomupendeza Mungu, anayewaalika kushiriki naye katika ufalme na utukufu wake.


Kwa mwisho, wandugu, sisi tumewafundisha namna gani munavyopaswa kuishi kusudi mupate kumupendeza Mungu. Na kweli, ni vile munavyoishi. Na sasa, tunawaomba na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu, muendelee mbele vizuri zaidi katika mwenendo ule.


Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ