Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 5:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Aliwaumba mwanaume na mwanamuke, kisha akawabariki na kuwapa jina “Wanadamu” siku ileile alipowaumba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 5:2
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akaumba mutu kwa mufano wake. Ndiyo, kwa mufano wake Mungu alimwumba. Aliwaumba mwanaume na mwanamuke.


Mungu akawabariki na kuwaambia: “Muzae, muongezeke, na mujaze inchi na kuitawala. Mutawale samaki wa bahari, ndege wa anga, na kila kiumbe chenye uzima kinachotembea katika dunia.”


Basi, Yawe Mungu akamutwaa yule mwanaume, akamuweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.


Halafu huyo mwanaume akasema: “Kweli! Huyu ni mufupa kutoka mifupa yangu, na nyama kutoka nyama yangu. Huyu ataitwa ‘Mwanamuke’, kwa sababu ametolewa katika mwanaume.”


Adamu alipokuwa na umri wa miaka mia moja na makumi tatu, alipata mutoto aliyefanana naye, na mwenye sura kama yake; akamwita Seti.


Mungu hakuwafanya ninyi wote wawili mukuwe mwili mumoja na roho moja? Alikusudia nini alipofanya hayo? Tuzae watoto wanaomupendeza Mungu. Kwa hiyo, muchunge uzima wenu na kuhakikisha kwamba hakuna hata mumoja wenu anayekosa uaminifu kwa muke wake.


Yesu akajibu: “Hamujasoma bado maneno yanayoandikwa katika Maandiko Matakatifu? ‘Kwa mwanzo Muumba aliumba mwanaume na mwanamuke,’


Lakini wakati Mungu alipowaumba watu wa kwanza, aliwaumba mwanaume na mwanamuke.


Kutokana na mutu mumoja, yeye aliumba watu wa mataifa yote kusudi waishi katika dunia yote. Aliwapangia nyakati na kukata mipaka ya inchi wanayopaswa kukaa ndani yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ