Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 49:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 “Wewe Yuda, wandugu zako watakusifu. Mukono wako utashika shingo la waadui zako, na wandugu zako watainama mbele yako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 49:8
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”


Lea akapata mimba tena, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Yuda, akisema: “Mara hii nitamusifu Yawe.” Kisha Lea akaacha kuzaa.


Wakati ule Yosefu alikuwa mukubwa kule Misri. Yeye ndiye aliyekuwa akiwauzishia wanainchi ngano. Basi, kaka zake wakakuja na kuinama mbele ya Yosefu kwa heshima.


Yuda na wana wake: Eri, Onani, Sela, Peresi na Zera. (Lakini Eri na Onani walikufa katika inchi ya Kanana). Wana wa Peresi walikuwa Hesironi na Hamuli.


Uliwakimbiza waadui zangu, na wale walionichukia niliwaangamiza.


Halafu Yoabu alimupelekea mufalme jumla ya watu. Katika inchi ya Israeli kulikuwa wanaume mashujaa elfu mia ine wenye ujuzi wa kutumia mapanga; na katika Yuda, kulikuwa wanaume elfu mia tano.


Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme Daudi kule Hebroni. Naye akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Israeli.


Lakini Yawe, Mungu wa Israeli, alinichagua mimi kati ya jamaa ya baba yangu kuwa mufalme wa Israeli kwa milele. Alichagua kabila la Yuda kusudi liongozeke; na kutokana na kabila lile, alichagua jamaa ya baba yangu, na kati ya wana wa baba yangu, alipendezwa nami na kuniweka nikuwe mufalme wa Israeli yote.


Ingawa kabila la Yuda ndilo lililokuja kuwa lenye nguvu zaidi kuliko mengine, na watawala walitoka mule, haki ya muzaliwa wa kwanza ilikuwa ya Yosefu).


Zera, Mwetiopia alishambulia inchi ya Yuda akiwa na jeshi la waaskari milioni moja na magari mia tatu, akasonga mbele mpaka Maresa.


Asa akakusanya watu wote wa Yuda na Benjamina, na wengine wote waliokuwa wakikaa katika inchi yake kutoka kabila la Efuraimu, la Manase na la Simeoni. Hawa walikuja kwake walipoona kwamba Yawe, Mungu wake yuko pamoja naye.


Aliweka majeshi katika miji yote ya inchi ya Yuda yenye kuta, na katika maeneo mengine ya Yuda akaweka waaskari walinzi, na katika miji ya Efuraimu ambayo baba yake Asa aliiteka.


Hata hivyo, watu wachache kati ya makabila ya Aseri, Manase na Zebuluni, walijinyenyekeza wakakuja Yerusalema.


Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Zaburi ya Asafu. Wimbo.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wote wataweza kuziona zambi zenu. Kila mutu atajua jinsi munavyokuwa na makosa. Kila kitendo munachotenda kinaonyesha zambi zenu. Ninyi mutapata azabu nami nitawatia katika mikono ya waadui zenu.


Wale waliokuwa chini ya bendera ya jeshi la kabila la Yuda, wakatangulia, kundi moja kisha lingine. Kiongozi wao alikuwa Nasoni mwana wa Aminadabu.


Kabila la Yuda lilikuwa na jamaa za Sela, Peresi, na Zera.


Hizo ndizo ukoo za Yuda, jumla wanaume elfu makumi saba na sita mia tano.


Juu ya kabila la Yuda akasema: “Ee Yawe usikilize kilio cha kabila la Yuda; umurudishe tena kwa wandugu zake. Upigane kwa mikono yako kwa ajili yake, usaidie kabila la Yuda mbele ya waadui zake.”


Na kule anangoja sasa mpaka waadui zake wote watiwe chini ya miguu yake.


Kwa maana inajulikana wazi kwamba Bwana wetu alitoka katika kabila la Yuda, na juu ya kabila lile Musa hakusema hata neno moja linaloelekea ukuhani.


Wafalme hao walipoletwa, Yoshua akawaita Waisraeli wote na wakubwa wa waaskari waliokwenda naye kwa vita, akawaambia: “Mukuje karibu muwakanyage wafalme hawa kwenye shingo yao.” Nao wakasogea na kuwakanyaga kwenye shingo.


Hii ndiyo inchi watu wa kabila la Yuda waliyopewa kulingana na ukoo zake. Miji iliyokuwa upande wa kusini kabisa wa inchi ya Yuda kuelekea mupaka wa Edomu ilikuwa: Kabuseli, Ederi, Yaguri, Kina, Dimona, Adada, Kedesi, Hazori, Itinani, Zifu, Telemu, Bealoti, Hazori-Hadata, Kerioti-Hesironi (ni kusema Hazori), Amamu, Sema, Molada, Hazari-Gada, Hesimoni, Beti-Peleti, Hazari-Suali, Beri-Seba, Biziotia, Bala, Iyimu, Ezemi, Eltoladi, Kesili, Horma, Ziklagi, Madimana, Sanisana, Lebaoti, Silhimu, Aini na Rimoni. Jumla ya miji makumi mbili na tisa pamoja na vijiji vyake. Miji iliyokuwa kwenye mabonde ilikuwa: Estaoli, Zora, Asina, Zanoa, Eni-Ganimu, Tapua, Enamu, Yarmuti, Adulamu, Soko, Azeka, Sarayimu, Aditaimu, Gedera na Gederotaimu. Jumla ya miji kumi na mine pamoja na vijiji vyake. Zenani, Hadaza, Migidali-Gadi, Dilani, Misipe, Yokiteli, Lakisi, Bozikati, Eguloni, Kaboni, Lamani, Kitilisi, Gederoti, Beti-Dagoni, Nama na Makeda. Jumla ya miji kumi na sita pamoja na vijiji vyake. Libuna, Eteri, Asani, Ifita, Asina, Nesibu, Keila, Akizibu na Maresa. Jumla ya miji tisa pamoja na vijiji vyake. Ekuroni pamoja na miji yake midogo na vijiji, Miji yote na vijiji vilivyokuwa karibu na Asidodi kati ya Ekuroni na bahari, Asidodi na Gaza pamoja na miji na vijiji vyake, mpaka kijito cha Misri mpaka pembeni ya bahari ya Mediteranea. Miji iliyokuwa kwenye eneo la milima ni: Samiri, Yatiri, Soko, Dana, Kiriati-Sana (au Debiri), Anabu, Estemoa, Animu, Goseni, Holoni na Gilo. Jumla ya miji kumi na mumoja pamoja na vijiji vyake. Arabu, Duma, Esani, Yanimu, Beti-Tapua, Afeka, Humuta, Kiriati-Arba (au Hebroni) na Siori. Jumla ya miji tisa pamoja na vijiji vyake. Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta, Yezereheli, Yokidamu, Zanoa, Kaina, Gibea na Timuna. Jumla ya miji kumi pamoja na vijiji vyake. Halihuli, Beti-Zuri, Gedori, Marati, Beti-Anoti na Eltekoni. Jumla ya miji sita pamoja na vijiji vyake. Kiriati-Bali, unaoitwa tena Kiriati-Yearimu, na Raba. Jumla ya miji miwili pamoja na vijiji vyake. Miji ya jangwa ilikuwa: Beti-Araba, Midini, Sekaka, Nibusani, Muji wa Chumvi na Engedi. Jumla ya miji sita pamoja na vijiji vyake.


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


Basi mumoja kati ya wale wazee akaniambia: “Usilie. Angalia, simba wa kabila la Yuda, wa uzao wa mufalme Daudi, amepata ushindi. Yeye anaweza kuvunja vile vifundo saba vya muhuri vya kizingo na kukifungua.”


Waisraeli wakaenda Beteli kuomba shauri kwa Mungu, wapate kujua kabila ambalo litakwenda kwanza kupigana na watu wa kabila la Benjamina. Yawe akataja kabila la Yuda liende kwanza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ