Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 49:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 lakini mimi sitashiriki mashauri yao mabaya. Ee roho yangu, usishiriki mikutano yao, maana, katika hasira yao, walimwua mutu, kwa mapenzi yao walikata mushipa wa ngombe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 49:6
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yakobo akamwambia Simeoni na Lawi: “Ninyi mumeniletea taabu kwa kunifanya nichukiwe na wakaaji wa inchi hii ya Wakanana na Waperizi. Mimi sina watu wengi, na kama wakikusanyika kwa kunishambulia wataniangamiza mimi pamoja na jamaa yangu.”


Daudi aliteka waaskari wapanda-farasi elfu moja na mia saba, na waaskari wa miguu elfu makumi mbili. Kisha Daudi alikata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wa magari ya vita, lakini aliacha farasi wa kutoshelea kwa magari mia moja.


Daudi akanyanganya magari ya vita elfu moja, waaskari wapanda-farasi elfu saba na wa miguu elfu makumi mbili. Kisha Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wa magari, lakini akaacha mia moja.


Heri mutu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi, wala kukusanyika na wenye kuzarau;


Zaburi ya Daudi. Ee nafsi yangu, umusifu Yawe; nafsi yangu yote isifu jina lake takatifu!


Heri, ee Mungu, ungewaua watu waovu! Heri wauaji wangeniondokea!


Kwa hiyo nitafurahi kwa moyo wote na kushangilia, nami nitakaa salama kabisa.


Usiniangamize pamoja na wenye zambi, wala usinitupe pamoja na wauaji,


Usiniazibu pamoja na watu wabaya, wale watenda maovu wanaosema vizuri na wenzao, kumbe wanajaa ubaya ndani ya moyo.


Wewe umegeuza malalamiko yangu kuwa ngoma ya furaha; umeniondolea huzuni yangu, ukanijaza furaha.


Nimepondekana kwa ajili ya matukano yao, wanaponiuliza kila siku: “Mungu wako, yupo wapi?”


Katika huzuni yangu, ninakumbuka jinsi nilivyokwenda na kundi la watu na kuwaongoza kwenda katika nyumba ya Mungu wakipiga vigelegele vya shukrani, kundi la watu likifanya sherehe!


Mbona ninahuzunika hivyo katika moyo? Kwa nini ninahangaika hivyo ndani mwangu? Nitamutumainia Mungu, nitamusifu tena yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.


Ndani ya vinywa vyao hamuna ukweli wowote; mioyo yao imejaa maangamizi, koo zao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu.


Moyo wangu ni tayari, ee Mungu, moyo wangu ni tayari; nitaimba na kukushangilia!


Ee Mungu, usikilize malalamiko yangu. Uyalinde maisha yangu kutoka vitisho vya waadui.


Wakisema: “Twende kuvizia mutu na kumwua; kuja tuwashambulie wasiokuwa na kosa!


Mawazo ya mwenye haki ni ya haki; mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.


Mimi sikuikaa pamoja na wanaojifurahisha, wala sikufurahi pamoja nao. Niliikaa peke yangu nikilemewa na nguvu yako; kwa maana ulinijaza hasira yako.


Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.


Kisha nitajisemesha hivi juu yangu mwenyewe: ‘Uko na mali nyingi ulizoweka akiba kwa miaka mingi. Sasa utulizane, ukule na kunywa na kujifurahisha.’


Musishirikiane pamoja na watu wasioamini. Kwa maana kuna ushirika gani kati ya haki na uovu? Kuna mapatano gani kati ya mwangaza na giza?


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayeua mutu kwa siri’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


Yoshua akakatakata mishipa ya miguu ya farasi wao wote na kuyateketeza magari yao kwa moto, kama Yawe alivyomwagiza.


Mafuriko ya muto Kisoni yaliwapeleka mbali, mafuriko makali ya muto Kisoni. Songa mbele kwa nguvu, ee nafsi yangu!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ