Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 49:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 “Wewe Rubeni ni muzaliwa wangu wa kwanza, nguvu yangu na tunda la ujana wangu. Wewe unawapita wandugu zako kwa ukubwa na nguvu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 49:3
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lea akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Rubeni, akisema: “Yawe ameona mateso yangu; bila shaka sasa mume wangu atanipenda.”


Wakati Israeli alipokuwa anakaa katika inchi ile, mwana wake Rubeni, akalala na Biliha, habara ya baba yake. Naye Israeli akasikia habari hizo. Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili.


Wana wa Lea walikuwa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Yakobo, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuluni.


Hawa ndio wazao wa Israeli ambao walikwenda Misri pamoja naye: Rubeni, muzaliwa wake wa kwanza,


Akamwambia baba yake: “Sivyo, baba! Huyu hapa ndiye muzaliwa wa kwanza. Tafazali, uweke mukono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”


Wana wa Israeli walikuwa: Rubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuluni,


Hawa ndio wazao wa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli. (Ingawa Rubeni alikuwa muzaliwa wa kwanza haki yake ya muzaliwa wa kwanza ilipewa kwa ndugu yake Yosefu kwa sababu Rubeni alilala na habara wa baba yake. Kwa hiyo, yeye hakutiwa katika hesabu ya ukoo kulingana na haki yake ya muzaliwa wa kwanza.


Wana wa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: Hanoki, Palu, Hesironi na Karmi.


Aliua wazaliwa wa kwanza katika inchi yao, ndilo chipukizi la kwanza la jamaa za Wamisri.


Aliwaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri; ndilo chipukizi la kwanza katika kambi la Hamu.


Eneo linalopakana na eneo la Efuraimu kutoka mashariki mpaka magaribi litakuwa la kabila la Rubeni.


Kwa kila kabila la Israeli, walihesabu watu kulingana na jamaa zao na ukoo zao. Waliandika majina ya kila mwanaume aliyekuwa na umri wa miaka makumi mbili na zaidi, aliyefaa kuingia katika jeshi. Hii ni hesabu yao kulingana na kabila yao. Kabila la Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli: elfu makumi ine na sita na mia tano. Kabila la Simeoni: elfu makumi tano na tisa na mia tatu. Kabila la Gadi: elfu makumi ine na tano mia sita na makumi tano. Kabila la Yuda: elfu makumi saba na ine na mia sita. Kabila la Isakari: elfu makumi tano na ine na mia ine. Kabila la Zebuluni: elfu makumi tano na saba mia ine. Kabila la Efuraimu: elfu makumi ine na mia tano. Kabila la Manase: elfu makumi tatu na mbili na mia mbili. Kabila la Benjamina: elfu makumi tatu na tano na mia ine. Kabila la Dani: elfu makumi sita na mbili na mia saba. Kabila la Aseri: elfu makumi ine na mumoja na mia tano. Kabila la Nafutali: elfu makumi tano na tatu na mia nane.


Kwanza ni kabila la Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Yakobo. Hanoki, Palu,


Anapaswa kukubali yule muzaliwa wa kwanza, mutoto wa yule mwanamuke asiyependwa, na kumupa haki yake: sehemu ya mali zake mara mbili.


Na makabila haya yatasimama juu ya mulima Ebali wakati laana zitakapotolewa: Rubeni, Gadi, Aseri, Zebuluni, Dani na Nafutali.


Musa akasema juu ya kabila la Rubeni: “Rubeni aishi wala asikufe, na watu wake wasikuwe wachache.”


“Umwandikie malaika wa kanisa la Laodikia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayeitwa ‘Amina’, mushuhuda mwaminifu, mwenye ukweli, na musingi wa viumbe vyote vya Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ