Mwanzo 49:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20023 “Wewe Rubeni ni muzaliwa wangu wa kwanza, nguvu yangu na tunda la ujana wangu. Wewe unawapita wandugu zako kwa ukubwa na nguvu. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Hawa ndio wazao wa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli. (Ingawa Rubeni alikuwa muzaliwa wa kwanza haki yake ya muzaliwa wa kwanza ilipewa kwa ndugu yake Yosefu kwa sababu Rubeni alilala na habara wa baba yake. Kwa hiyo, yeye hakutiwa katika hesabu ya ukoo kulingana na haki yake ya muzaliwa wa kwanza.
Kwa kila kabila la Israeli, walihesabu watu kulingana na jamaa zao na ukoo zao. Waliandika majina ya kila mwanaume aliyekuwa na umri wa miaka makumi mbili na zaidi, aliyefaa kuingia katika jeshi. Hii ni hesabu yao kulingana na kabila yao. Kabila la Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli: elfu makumi ine na sita na mia tano. Kabila la Simeoni: elfu makumi tano na tisa na mia tatu. Kabila la Gadi: elfu makumi ine na tano mia sita na makumi tano. Kabila la Yuda: elfu makumi saba na ine na mia sita. Kabila la Isakari: elfu makumi tano na ine na mia ine. Kabila la Zebuluni: elfu makumi tano na saba mia ine. Kabila la Efuraimu: elfu makumi ine na mia tano. Kabila la Manase: elfu makumi tatu na mbili na mia mbili. Kabila la Benjamina: elfu makumi tatu na tano na mia ine. Kabila la Dani: elfu makumi sita na mbili na mia saba. Kabila la Aseri: elfu makumi ine na mumoja na mia tano. Kabila la Nafutali: elfu makumi tano na tatu na mia nane.