Wachuuzi Wamidiani walipofika pahali pale, wale wandugu wakamwondoa Yosefu katika shimo, wakamwuzisha kwa Waisimaeli kwa bei ya vikoroti makumi mbili vya feza; nao wakamupeleka Yosefu Misri.
Kisha wakasemezana wao kwa wao: “Kweli sisi tulimukosea ndugu yetu. Ingawa tulimwona katika taabu, hatukumujali hata alipotusihi. Ndiyo maana taabu hii yote inatupata.”
Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”
Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”