2 “Mukusanyike musikie, enyi wana wa Yakobo, munisikilize mimi Israeli, baba yenu.
“Wewe Rubeni ni muzaliwa wangu wa kwanza, nguvu yangu na tunda la ujana wangu. Wewe unawapita wandugu zako kwa ukubwa na nguvu.
Hata simba wakali wanakosewa na kusikia njaa, lakini wanaomutafuta Yawe hawakosewi chochote kizuri.
Mukuje, enyi vijana munisikilize, nami nitawafundisha kumwabudu Yawe.
Umusikilize baba yako aliyekuzaa, wala usimuzarau mama yako akizeeka.
Mwana wangu, unisikilize kwa uangalifu, ufuate mwenendo wa maisha yangu.
Mwana wangu, sikia hekima yangu, tega sikio usikie elimu yangu.
Mwana wangu, shika amri za baba yako, wala usisahau mashauri ya mama yako;
Mwana wangu, ushike maneno yangu, uchunge amri zangu.
Sasa wana wangu, munisikilize; mutege sikio kwa maneno ya kinywa changu.
“Sasa basi, wana wangu, munisikilize: heri wale wanaofuata njia zangu.
Mukusanyike wote musikilize! Nani kati yenu alitabiri vitu hivi? Yule ambaye Yawe anamupenda atatimiza mapenzi yake juu ya Babeli, atawashambulia Wakaldea.