Mwanzo 49:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200219 “Gadi atashambuliwa na wanyanganyi, lakini yeye atawafuata nyuma na kuwashambulia. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Kutoka kabila la Gadi, hawa ndio waaskari mashujaa na walioelewa sana vita. Wakatoka kwao kwenda kujiunga na kundi la Daudi alipokuwa katika maficho kule katika jangwa. Walikuwa hodari wa kutumia mikuki na ngao, wenye nyuso za kuogopesha kama za simba, na katika milima walikuwa wepesi wa kukimbia kama swala. Kiongozi wao mukubwa alikuwa Ezeri. Alifuatwa na: Obadia, Eliabu, Misimana, Yeremia, Atai, Elieli, Yohana, Elisabadi, Yeremia, Makibanai.
Basi, Mungu wa Israeli akasukuma roho ya Puli, mufalme wa Asuria, (ambaye alijulikana vilevile kwa jina la Tiglati-Pileseri), akashambulia inchi yao na kuwapeleka watu wa kabila la Rubeni, la Gadi na nusu ya kabila la Manase kwa upande wa mashariki mpaka uhamisho kule Hala, Habori na Hara, pembeni ya muto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.