Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 49:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 49:10
58 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu na kiti chake cha kifalme cha ufalme wake nitakiimarisha milele.


Ukoo wako na ufalme wako vitadumu imara siku zote. Kiti chako cha kifalme kitakuwa imara milele.”


Hii ndiyo hesabu ya makundi ya waaskari wenye silaha waliojiunga na Daudi kule Hebroni kwa kumutwalia ufalme kutoka kwa Saulo, kulingana na neno la Yawe:


Waaskari hao wote, waliojitayarisha kabisa kwa vita, walikwenda Hebroni na nia yao kubwa ikiwa ni kumuweka Daudi kuwa mufalme wa inchi yote ya Israeli. Nao watu wote wa Israeli, wakaungana wakiwa na nia moja ya kumuweka Daudi kuwa mufalme.


Mungu amesema toka hekalu lake takatifu: “Sasa nitakwenda kwa shangwe kugawanya Sekemu, bonde la Sukoti nitalipima sehemu sehemu.


Uwaponyeshe hao watu unaowapenda! Utuokoe kwa mukono wako! Utusikilize!


Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu; Efuraimu ni kofia yangu ya chuma, na Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.


Lakini alichagua kabila la Yuda, mulima Sayuni anaoupenda.


Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


Simama, ee Sayuni uangaze; maana mwangaza unatokea kwa ajili yako, utukufu wa Yawe unakuangazia.


Yawe ametangaza katika dunia yote, muwaambie watu wa Sayuni hivi: Mukombozi wenu anakuja, yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Mwongozi wao atakuwa mumoja wao, mutawala wao atatokea katikati yao. Nitamuruhusu kuwa karibu nami; maana, ni nani anayeweza kusubutu kuhatarisha uzima wake kwa kunikaribia? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Basi, ndivyo inavyokuwa vilevile: sitawatupa wazao wa Yakobo na Daudi, mutumishi wangu; nitamuchagua mumoja kati ya wazao wake atawale wazao wa Abrahamu, Isaka na Yakobo. Kwa maana nitawarudishia tena hali yao na kuwahurumia.


Ulikuwa na matawi yenye nguvu, ambayo yalikuwa fimbo za kifalme. Muzabibu huo ulikomaa kupita miti mingine, watu walisifu ukubwa wa shina lake na wingi wa matawi yake.


Lakini moto umetoka kwenye shina lake, ukayateketeza matawi na matunda yake. Matawi yake hayatakuwa na nguvu hata kidogo, wala hayatakuwa fimbo za kifalme. Huo umekuwa wimbo wa maombolezo; ndivyo unavyoimbwa siku zote.


Mushale ulioangukia kwa upande wa mukono wake wa kuume, ulionyesha Yerusalema. Pale wataweka vifaa vya vita kwa kuubomoa. Anaamuru mauaji, kelele za vita zipigwe, vifaa vya vita kwa kubomoa milango viwekwe, lundo ya udongo na minara kwa kuushambulia muji viwekwe vilevile.


Uharibifu! Uharibifu! Hakuna chochote katika muji huu nitakachoacha. Lakini mbele ya hayo kutafika kwanza yule ambaye nimemupa mamlaka ya kuuazibu, ambaye mimi nitamupa muji ule.


Basi, ujue na kufahamu jambo hili: tangu wakati amri itakapotolewa ya kujengwa upya Yerusalema mpaka kuja kwa yule aliyepakwa mafuta, yule anayekuwa mukubwa, ni muda wa majuma saba. Kwa muda wa majuma makumi saba na mawili, Yerusalema utajengwa upya, wenye barabara kubwa na kuta, lakini wakati huo utakuwa wa taabu.


Yawe anasema hivi: Lakini wewe Betelehemu katika Efurata, wewe ni mudogo tu kati ya ukoo wa Yuda, lakini kwako kutanitokea mutawala atakayetawala juu ya Israeli. Asili yake ni ya zamani sana.


Nitayatikisa mataifa yote na mali zao zote zitaletwa humu, nami nitaifanya nyumba hii kuwa yenye utukufu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Watapitia katika bahari ya mateso, nami nitayapiga mawimbi yake, na vilindi vya maji ya muto Nili vitakauka. Kiburi cha Asuria kitavunjwa na nguvu za Misri zitatoweka.


Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!


Kisima kilichochimbwa na wakubwa kilichochimbwa sana na wenye cheo, kwa fimbo zao za utukufu na bakora. Kutoka katika jangwa wakasafiri mpaka Matana,


Ninamwona atakayekuja, ninamwona, lakini hayuko karibu. Nyota itatokea kwa wazao wa Yakobo, atatokea mufalme kati ya Waisraeli. Kwa fimbo yake atapiga viongozi wa Wamoabu, atawaangamiza wazao wote wa Seti.


Mumoja wa wazao wa Yakobo atatawala naye atawaangamiza watakaobaki katika muji.


Yeye atazaa mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yesu, kwa maana ndiye atakayewaokoa watu wake toka katika zambi zao.”


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Nalo kundi la watu waliomutangulia Yesu na lile la watu waliofuata nyuma yake, wakaanza kulalamika, wakisema: “Usifiwe wewe Mwana wa Daudi! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana! Mungu asifiwe juu mbinguni!”


Mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atayatenga kwa makundi mawili kama vile muchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi.


Lakini mimi, nitakaponyanyuliwa toka katika dunia, nitawavuta watu wote kuja kwangu.”


Pilato akawaambia: “Ninyi wenyewe mumukamate na mumuhukumu kufuatana na sheria yenu.” Wakamujibu: “Sisi hatuna ruhusa ya kuua mutu.”


Tokea saa ile Pilato alitafuta njia ya kumufungua Yesu. Lakini Wayuda wakapiga kelele, wakisema: “Ukimufungua mutu huyu, wewe si rafiki wa Mufalme wa Roma. Kila mutu anayejifanya kuwa mufalme, anamupinga Mufalme wa Roma!”


Lakini wakapiga kelele wakisema: “Umwue! Umwue! Umutundike juu ya musalaba!” Pilato akawauliza: “Munataka nimutundike mufalme wenu juu ya musalaba?” Wakubwa wa makuhani wakajibu: “Sisi hatuna mufalme mwingine isipokuwa Mufalme wa Roma.”


na kumwambia: “Kwenda unawe uso katika kisima cha Siloamu” (maana ya jina hili ni “Aliyetumwa”). Basi yule kipofu akaenda na kunawa uso, akarudi akiwa mwenye kuona.


Isaya naye anasema: “Muzao wa Yese atatokea, atatawala watu wa mataifa, nao watamutumainia.”


Kwa maana sisi wote tunapaswa kusimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Kristo, kusudi kila mutu alipwe kufuatana na matendo yake mema au mabaya aliyofanya alipokuwa akiishi ndani ya mwili wake.


atakula mutoto wake muchanga kwa siri nyuma ya kumuzaa pamoja na nyama ya kizazi kwa sababu ya ukosefu wa chakula.


Kwa maana inajulikana wazi kwamba Bwana wetu alitoka katika kabila la Yuda, na juu ya kabila lile Musa hakusema hata neno moja linaloelekea ukuhani.


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ