Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 49:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yakobo akawaita wana wake, akasema: “Mukusanyike pamoja niwaambie mambo yatakayowapata siku zinazokuja.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 49:1
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Musiwaguse wachaguliwa wangu; musiwazuru manabii wangu!”


Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu; yeye anawajulisha agano lake.


Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


Yawe wa majeshi alinifunulia haya akisema: Hakika uovu huu hautasahauliwa mbele ya kufa kwenu. Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Siku zinakuja ambapo vyote vinavyokuwa katika nyumba yako na vitu vyote babu zako walivyokusanya mpaka leo, vitapelekwa Babeli. Hakuna kitu chochote kitakachobaki. –Ni Yawe anayesema hivyo.–


Mukusanyike wote musikilize! Nani kati yenu alitabiri vitu hivi? Yule ambaye Yawe anamupenda atatimiza mapenzi yake juu ya Babeli, atawashambulia Wakaldea.


Ni nani aliyeamini mambo tuliyoyasikia? Mukono wa Mungu umefunuliwa kwa ajili ya nani?


Hasira ya Yawe haitatulia, mpaka atakapotimiza na kukamilisha mapenzi ya moyo wake. Kutakuja siku ambapo mutaelewa vema mambo hayo.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Kiro wa Persia, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, alipewa ufunuo. Ufunuo huo ulikuwa wa kweli, lakini ulikuwa mugumu sana. Hata hivyo alielewa ufunuo huo maana alifahamu maono vilevile.


nami nimekuja kukusaidia upate kuyafahamu mambo yatakayowapata watu wako wakati unaokuja, maana maono uliyoona yanaelekea wakati unaokuja.


Mufalme akamwambia Danieli: Hakika, Mungu wako ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme, na ndiye anayefumbua mafumbo kwa sababu ameweza kunifumbulia fumbo hili.


Hakika, Bwana wetu Yawe hafanyi kitu bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.


Kutakuja wakati ambapo mulima wa nyumba ya Yawe utakuwa mukubwa kuliko milima yote. Utanyanyuliwa juu ya vilima vyote. Watu wengi watakimbilia kule,


Sasa ninarudi kwa watu wangu, lakini mbele sijaondoka, acha nikuambie mambo ambayo watu hao watawatendea watu wako siku zinazokuja.


alikuwa amemufunulia kwamba hatakufa mbele hajamwona Kristo wa Bwana.


‘Mungu anasema: Katika siku za mwisho, nitashusha Roho wangu juu ya watu wote; wana wenu na wabinti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono nao wazee wenu wataota ndoto.


Mutakusanya wanaume, wanawake, watoto na wageni wanaoishi katika miji yenu, kusudi kila mumoja asikie maneno haya ya kujifunza kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kuwa waangalifu kushika maneno ya sheria hii.


Mambo haya yote yatakapowapata huko, kisha mukipata taabu, mutamurudilia Yawe na kumutii.


Roho Mutakatifu anasema wazi kwamba katika nyakati za mwisho, watu wengine watapotoka katika imani yao na kufuata roho za udanganyifu na mafundisho ya pepo.


Ujue vizuri kwamba siku za mwisho zitakuwa nyakati za magumu.


Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.


Nyuma ya mambo hayo nilipata maono mengine. Niliona mulango mumoja umefunguliwa wazi mbinguni. Halafu ile sauti niliyosikia mara ya kwanza, iliyolia kama baragumu, ikaniambia: “Panda huku, nami nitakuonyesha mambo yanayopaswa kutokea nyuma ya hayo ya mbele.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ