Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 48:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Yosefu akamujibu baba yake: “Hawa ni wana wangu Mungu alionijalia nikiwa huku.” Israeli akasema: “Tafazali, uwalete karibu nipate kuwabariki.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 48:9
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu unitengenezee chakula kitamu, kile ninachopenda, uniletee nikule, nipate kukubariki mbele ya kufa kwangu.”


Yakobo akamukasirikia Rakeli na kumwambia: “Mimi nimekuwa pahali pa Mungu aliyekuzuia kupata watoto?”


Esau alipoinua macho na kuwaona wale wamama na watoto, akauliza: “Ni wa nani hawa unaokuwa nao?” Yakobo akamujibu: “Hawa ni watoto ambao Mungu, kwa neema yake, amenijalia mimi mutumishi wako.”


Hayo ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hayo ndiyo maneno baba yao aliyowaambia alipowabariki, kila mumoja wao kama alivyostahili.


Mungu alimupatia Hemani aliyekuwa akitabiria mufalme, wana hawa kumi na wane, na wabinti watatu, kama vile alivyoahidi kwa kumutukuza.


Watoto ni urizi kutoka kwa Yawe; uzao ni zawadi yake kwetu sisi.


Mimi pamoja na watoto Yawe alionipa ni kitambulisho na mufano katika Israeli kwa jina la Yawe wa majeshi anayekaa kwenye mulima Sayuni.


Hii ndiyo baraka ambayo Musa, mutu wa Mungu aliwatakia Waisraeli mbele ya kufa kwake. Alisema hivi:


Kwa njia ya imani, Yakobo alipokuwa karibu kufa, alibariki kila mumoja wa wana wa Yosefu; akainama kwa kumwabudu Mungu akiegemea fimbo yake.


Hivyo Hana akapata mimba, akazaa mutoto wa kiume. Hana akamwita mutoto huyo Samweli, maana alisema: “Nimemwomba kwa Yawe.”


Nilimwomba anipe mutoto huyu, na yeye alinipa kile nilichomwomba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ