Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 48:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Yakobo akaendelea kusema: “Wana wako wawili uliowapata hapa Misri mbele sijafika, ni wana wangu. Efuraimu na Manase watakuwa wangu kama vile Rubeni na Simeoni wanavyokuwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 48:5
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kule Misri, Asenati binti ya Potifera, aliyekuwa kuhani wa muji wa Oni, alimuzalia Yosefu wana wawili: Manase na Efuraimu.


Nyuma ya mambo hayo, Yosefu akapewa habari kwamba baba yake ni mugonjwa. Hivyo, akatwaa wana wake wawili, Manase na Efuraimu, akakwenda nao kwa baba yake.


Lakini, watoto utakaopata nyuma watakuwa wako, kwa jina la wandugu zao wataitwa katika urizi wao.


Kwa mukono wako wa kuume uliwakomboa watu wako; uliwakomboa wazao wa Yakobo na Yosefu.


Yawe aliyewaumba enyi watu wa Yakobo, yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, anasema hivi: Musiogope, maana mimi nimewakomboa; nimewaita kwa jina lenu nanyi ni wangu.


Nilipopita tena karibu nawe, nikakuona. Wakati huu, ulikuwa umefikia umri wa kupendwa kama binti. Nikalitandaza vazi langu juu yako na kuufunika uchi wako. Nikafanya nawe agano la ndoa, nawe ukakuwa wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Hii ndiyo mipaka ya inchi mutakayoigawanyia makabila kumi na mawili ya Waisraeli. Lakini kabila la Yosefu lipewe mara mbili.


Kwa sababu mimi Yawe ni mutakatifu, nami nimewatenga ninyi na mataifa mengine kusudi mukuwe mali yangu, mutakuwa watakatifu.


Kisha Yawe wa majeshi akasema hivi: Hao watakuwa watu wangu. Watakuwa urizi wangu wa kipekee siku ile nitakaposimama kufanya jambo ninalokusudia. Sitawazuru kama vile baba asivyomuzuru mwana wake anayemutumikia.


Nitakuwa Baba yenu nanyi mutakuwa wana na wabinti wangu. Ni mimi Bwana Mwenye Uwezo ninayesema.”


Mungu amekusudia tangu zamani kutukubali sisi kuwa watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Alifanya vile kufuatana na mapenzi yake.


Kwa njia ya imani, Yakobo alipokuwa karibu kufa, alibariki kila mumoja wa wana wa Yosefu; akainama kwa kumwabudu Mungu akiegemea fimbo yake.


Utayagawanyia inchi hizo makabila kenda na nusu ya kabila la Manase ambao bado hawajapata kitu.”


Wazao wa Yosefu walikuwa makabila mawili: Manase na Efuraimu. Kabila la Lawi halikupewa sehemu yoyote ya inchi, lakini miji tu ya kuishi na mashamba ya malisho kwa ajili ya nyama wao na riziki zao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ