Yosefu alipoona kwamba baba yake ameuweka mukono wake wa kuume juu ya kichwa cha Efuraimu hakupendezwa. Basi, akaushika mukono wa baba yake, akitaka kuuondoa juu ya kichwa cha Efuraimu auweke juu ya kichwa cha Manase.
Lakini baba yake akakataa, akisema: “Ninajua, mwana wangu, ninajua. Wana wa Manase vilevile watakuwa taifa na wakubwa. Hata hivyo, ndugu yake mudogo atakuwa mukubwa kuliko yeye na wazao wake watakuwa mataifa mengi.”
Lakini Petro akajibu: “Hapana, hata kidogo Ee Bwana! Mimi sijakula bado kitu chochote kisichoruhusiwa kukuliwa, wala chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu.”
Lakini nikajibu: ‘Hapana, hata kidogo, ee Bwana! Ndani ya kinywa changu hamujaingia bado kitu chochote kisichoruhusiwa kukuliwa wala chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu.’