Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 48:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote, awabariki vijana hawa! Jina langu na majina ya babu zangu, Abrahamu na Isaka, yadumishwe katika vijana hawa; nao waongezeke kwa wingi katika dunia.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 48:16
46 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini malaika wa Yawe akamwita kutoka mbinguni: “Abrahamu! Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa!”


Malaika wa Yawe akamwita Abrahamu mara ya pili kutoka mbinguni,


Naye akamwuliza: “Jina lako nani?” Yeye akamujibu: “Yakobo.”


Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako. Usiogope kwenda Misri. Utakapokuwa kule, nitakufanya kuwa taifa kubwa.


Yakobo akaendelea kusema: “Wana wako wawili uliowapata hapa Misri mbele sijafika, ni wana wangu. Efuraimu na Manase watakuwa wangu kama vile Rubeni na Simeoni wanavyokuwa.


“Yosefu ni kama muti unaozaa, muti unaozaa kando ya chemichemi, matawi yake yanatanda kwenye ukuta.


Lakini Daudi akamujibu Rekabu na ndugu yake Bana, wana wa Rimoni wa Beroti: “Kama vile Yawe anavyoishi, yeye ameyakomboa maisha yangu kutoka kila adui.


Halafu mufalme aliapa, akisema: “Kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyekomboa roho yangu katika taabu nyingi,


kama watu wangu hao wakijinyenyekeza, wakiomba, wakinitafuta na kuacha njia zao mbaya, basi, mimi nitawasikiliza kutokea juu mbinguni, nitawasamehe zambi yao na kustawisha inchi yao.


Yawe atakukinga na uovu wote; atayalinda salama maisha yako.


Nitamutukuza Yawe nyakati zote, sitaacha hata kidogo kutaja sifa zake.


Ubaya unawaletea waovu kifo; wanaowachukia watu wa haki wataazibiwa.


Masikini alimulilia Yawe, naye akamusikia, na kumwokoa katika taabu zake zote.


Malaika wa Yawe anawalinda wote wanaomwabudu, na kuwaokoa kutoka katika hatari.


Lakini wazao wa Israeli wakaongezeka sana, wakakuwa wengi na wenye nguvu sana, wakaenea kila pahali katika inchi ya Misri.


Mukombozi wetu ndiye Mutakatifu wa Israeli; Yawe wa majeshi ndilo jina lake.


Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.


Namna gani unakuwa kama mutu aliyechanganyikiwa, kama shujaa asiyeweza kusaidia mutu? Ingawa hivyo wewe ee Yawe unakaa katikati yetu; nasi tunajulikana kwa jina lako, usituache.


Nitakuokoa toka katika mikono ya watu waovu, na kukuopoa toka katika makucha ya watesaji.


Nao Waisraeli watarizi mabaki ya inchi ya Edomu na mataifa yote yaliyokuwa yangu. –Ni ujumbe wa Yawe, yule anayefanya hivyo.


Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.


ilikuwa watu elfu mia sita na tatu na mia tano makumi tano.


Usituache kuanguka katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. [Kwa maana ufalme, uwezo na utukufu ni vyako hata milele. Amina.]’


Sikuombi kama uwaondoe katika dunia, lakini ninakuomba uwakinge na yule Mwovu Shetani.


kusudi watu wote wengine wamugeukie Bwana, watu wa mataifa yote wapate kuwa watu wangu wa pekee.


Na si viumbe hivi tu; hata sisi tuliokwisha kuwa na Roho wa Mungu kama sehemu ya kwanza ya zawadi Mungu atakazotoa, tunaugua vilevile ndani yetu, tukingojea kukubaliwa na Mungu kuwa watoto wake, maana yake kukombolewa kwa kimwili.


Wote walikunywa kinywaji kimoja cha kiroho; kwa maana walikunywa maji yaliyotoka ndani ya lile jiwe lililosafiri pamoja nao, nalo jiwe lilikuwa Kristo.


Vilevile tusimupime Bwana kama vile wamoja wao walivyofanya, hata wakauawa na nyoka.


Mataifa yote katika dunia yakiona kwamba ninyi munaitwa kwa jina la Yawe yatawaogopa.


Utukufu wake ni utukufu wa ngombe dume wa kwanza, pembe zake ni za mbogo dume. Atazitumia kusukuma mataifa; yote atayasukuma mpaka miisho ya dunia. Efuraimu atakuwa na pembe hizo elfu kumi na Manase kwa maelfu.”


Bwana ataniokoa toka katika mambo yote mabaya na kunipeleka salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Bwana atukuzwe milele na milele. Amina.


Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.


Kwa njia ya imani, Yakobo alipokuwa karibu kufa, alibariki kila mumoja wa wana wa Yosefu; akainama kwa kumwabudu Mungu akiegemea fimbo yake.


Basi, Yoshua akawaambia wazao wa Yosefu, ni kusema kabila la Efuraimu na Manase: “Kweli ninyi mumekuwa wengi na wenye uwezo mukubwa. Haifai mupate sehemu moja tu,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ