Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 48:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Lakini Israeli akaipishanisha mikono yake: mukono wake wa kuume akauweka juu ya kichwa cha Efuraimu, ingawa alikuwa mudogo na mukono wake wa kushoto akauweka juu ya kichwa cha Manase, aliyekuwa muzaliwa wa kwanza.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 48:14
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yosefu akamwita mwana wake wa kwanza Manase, akisema: “Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote na jamaa ya baba yangu.”


Mwana wake wa pili akamwita Efuraimu, akisema: “Mungu amenipa watoto katika inchi ya mateso yangu.”


Kule Misri, Asenati binti ya Potifera, aliyekuwa kuhani wa muji wa Oni, alimuzalia Yosefu wana wawili: Manase na Efuraimu.


Yosefu akawainua wana wake wawili, Efuraimu katika mukono wake wa kuume, akimwelekeza kwenye mukono wa kushoto wa baba yake, na Manase katika mukono wake wa kushoto, akimwelekeza kwenye mukono wa kuume wa baba yake, akawasogeza kwa babu yao.


Yosefu alipoona kwamba baba yake ameuweka mukono wake wa kuume juu ya kichwa cha Efuraimu hakupendezwa. Basi, akaushika mukono wa baba yake, akitaka kuuondoa juu ya kichwa cha Efuraimu auweke juu ya kichwa cha Manase.


Akamwambia baba yake: “Sivyo, baba! Huyu hapa ndiye muzaliwa wa kwanza. Tafazali, uweke mukono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”


Zaburi ya Daudi. Yawe anamwambia bwana wangu: “Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”


Mukono wa nguvu wa Yawe umeleta ushindi! Mukono wa Yawe umetenda mambo makubwa!”


“Mukono wako wa kuume, ee Yawe, unatukuka kwa nguvu; kwa mukono wako wa kuume, ee Yawe, unawaponda waadui.


Kwa upande wa magaribi, wale wanaokuwa chini ya bendera ya kundi la Efuraimu watapiga kambi kulingana na jeshi lake kiongozi wao akiwa Elisama mwana wa Amihudi,


Utakapowaleta Walawi mbele yangu, Waisraeli watawawekea Walawi mikono.


Sasa ninawatwaa Walawi pahali pa wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli,


Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.


Watu wamoja walimuletea Yesu watoto kusudi awawekee mikono na kuwaombea, lakini wanafunzi wakawakaripia watu wale.


Naye alipokwisha kuweka mikono juu yao, akaondoka pale.


“Munapoomba, musikuwe kama wanafiki, kwa maana wanapenda kuomba wakisimama katika nyumba za kuabudia na pembeni ya barabara, kusudi wapate kujionyesha mbele ya watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


Halafu akaweka mikono juu yake kwa kumuponyesha. Na mara moja akainuka tena, na kumutukuza Mungu.


Jua lilipotua, wakamuletea Yesu watu wote wenye kuwa na magonjwa mbalimbali. Akaweka mikono yake juu ya kila mumoja wao, akawaponyesha.


Basi wakafunga tena kula chakula na kuomba. Kisha wakaweka mikono juu yao na kuwatuma waende safari.


Kisha wakawaweka mbele ya mitume, nao wakaomba na kuweka mikono juu yao.


Yoshua mwana wa Nuni akajaa roho ya hekima, kwa sababu Musa alikuwa amemuwekea mikono yake. Hivyo Waisraeli wakamutii Yoshua na kufuata amri ambazo Yawe alimupa Musa.


Usiache kutumia ile zawadi ya kiroho inayokuwa ndani yako, uliyopokea kutokana na maneno ya manabii na kwa njia ya kuwekewa mikono na wazee wa kanisa.


Usiweke mikono juu ya mutu kwa haraka, wala usishiriki zambi za watu wengine. Ujilinde wewe mwenyewe katika maisha safi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ