Alipoinua macho yake, akaona watu watatu wakisimama mbali kidogo mbele yake. Mara tu alipowaona, akakimbia kutoka kwenye mulango wa hema yake, akakwenda kuwapokea. Alipowafikia akainama kwa heshima
Wale wamalaika wawili wakafika katika muji wa Sodoma magaribi. Loti alikuwa ameketi kwenye mulango wa muji wa Sodoma. Alipowaona, akasimama kwenda kuwapokea, akainama kwa heshima.
Wakati ule Yosefu alikuwa mukubwa kule Misri. Yeye ndiye aliyekuwa akiwauzishia wanainchi ngano. Basi, kaka zake wakakuja na kuinama mbele ya Yosefu kwa heshima.
Yosefu akawainua wana wake wawili, Efuraimu katika mukono wake wa kuume, akimwelekeza kwenye mukono wa kushoto wa baba yake, na Manase katika mukono wake wa kushoto, akimwelekeza kwenye mukono wa kuume wa baba yake, akawasogeza kwa babu yao.
Basi, Batiseba akamwendea mufalme Solomono kwa kumwelezea ombi la Adonia. Mufalme akasimama kwenda kumupokea mama yake, akainama mbele yake. Halafu, akaikaa katika kiti chake cha kifalme, akaagiza mama yake aletewe kiti, naye akaikaa kwa upande wa kuume wa mufalme.