Kwa hiyo uniapie kwa jina la Mungu kwamba hautanidanganya mimi au watoto wangu au wazao wangu. Kadiri mimi nilivyokutendea mema, vivyo hivyo nawe unitendee mema mimi na inchi hii unamokaa.”
Wakati wa kufa kwake ulipokaribia, Yakobo akamwita mwana wake Yosefu, akamwambia: “Sasa, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, weka mukono wako chini ya mapaja yangu, uniahidi kwamba utanitendea kwa wema na uaminifu. Usinizike huku Misri,
‘Mimi niko karibu kufa. Inakupasa kunizika katika kaburi nililojichongea katika inchi ya Kanana.’ Kwa hiyo ninamwomba aniruhusu niende kumuzika baba yangu, kisha nitarudi.”
Zaidi ya hayo, watumishi wa mufalme walikuja kumupa pole bwana wetu mufalme Daudi wakisema: ‘Mungu wako alifanye jina la Solomono kuwa lenye sifa kuliko lako; tena akitukuze kiti chake cha kifalme kuliko kiti chako.’ Halafu mufalme akainama juu ya kitanda