Esau akasema: “Heri nikuachie sehemu ya watu wangu.” Lakini Yakobo akasema: “Kuna sababu gani ya kufanya hivyo? Inanitosha kwamba mimi nimepata kukubaliwa mbele yako, ewe bwana wangu.”
Mufalme akamupa Yosefu jina la Kimisri: Safenati-Panea. Akamupa Asenati, binti ya Potifera, kuhani wa muji wa Oni kuwa muke wake. Basi, Yosefu akaanza kutembelea inchi nzima ya Misri.
Wakati wa mavuno, sehemu moja ya tano mutamupa mufalme. Sehemu ine zitakazobaki zitakuwa mbegu na chakula kwa ajili yenu na jamaa zenu na watoto wenu.”
Ndivyo Yosefu alivyotangaza sheria moja ambayo iko mpaka leo katika inchi ya Misri. Kila mwanainchi anapaswa kutoa sehemu moja ya tano ya mavuno yake kwa mufalme. Udongo wa makuhani tu ndio haukununuliwa na kufanywa mali ya mufalme.
Ruta akamujibu: “Bwana, wewe umenifanyia wema mukubwa sana. Ingawa mimi si kama mumoja wa watumishi wako, nimetosheka kwa sababu umenifariji sana na kuongea nami kwa upendo.”