Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 47:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Kisha Yosefu akawaambia watu: “Muangalie, nimekwisha kuwanunua ninyi wote na mashamba yenu kuwa mali ya mufalme. Mutapewa mbegu nanyi mutapanda mashamba yenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 47:23
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wale ngombe saba waliokonda sana, ambao waliwafuata wale wanono, na yale masuke matupu saba, yaliyokaushwa na upepo mukali wa jangwa, maana yake ni miaka saba ya njaa.


Huu ni mwaka wa pili tu wa njaa katika inchi, na kungali miaka mitano zaidi ambapo watu hawataweza kulima wala kuvuna mavuno.


Udongo ambao Yosefu hakununua ni ule iliokuwa wa makuhani. Hao hawakulazimika kuuzisha udongo wao maana waliishi kwa posho waliyopewa na mufalme.


Wakati wa mavuno, sehemu moja ya tano mutamupa mufalme. Sehemu ine zitakazobaki zitakuwa mbegu na chakula kwa ajili yenu na jamaa zenu na watoto wenu.”


Mutu muzuri anakopesha bila faida; anafanya shuguli zake kwa kutumia haki.


Watu wanamulaani mutu anayeficha ngano, lakini wanamutakia baraka mwenye kuiuzisha.


Mulimaji mwenye bidii ana chakula tele, lakini anayefuata mambo yasiyofaa hana akili.


Shamba la masikini linatoa mazao mengi, lakini linanyanganywa juu ya wale wanaopotosha haki.


Panda mbegu asubui na usiache kupanda mpaka magaribi, maana, haujui mbegu gani zitaota; za asubui, za magaribi, au zote zitakuwa nzuri.


Kama vile mvua na teluji inavyoshuka toka mbinguni, wala hairudi kule lakini inalowanisha udongo, kuuzalisha na kuchipukiza mimea, na kumupatia mupandaji mbegu na kuwapa watu chakula,


“Basi ni nani anayekuwa mutumishi mwaminifu na mwenye akili? Ni yule bwana wake aliyemuweka kuwa musimamizi wa watumishi wake wengine na kumwamuru kuwapatia posho yao kwa wakati uliopangwa.


Mungu ndiye anayemupatia mupandaji mbegu na mukate wa kukula. Kwa hiyo atawapatia ninyi mbegu yoyote munayohitaji na kuiotesha, kusudi moyo wenu wa kutoa upate kuzaa matunda mengi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ