Mwanzo 47:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
23 Kisha Yosefu akawaambia watu: “Muangalie, nimekwisha kuwanunua ninyi wote na mashamba yenu kuwa mali ya mufalme. Mutapewa mbegu nanyi mutapanda mashamba yenu.
Wale ngombe saba waliokonda sana, ambao waliwafuata wale wanono, na yale masuke matupu saba, yaliyokaushwa na upepo mukali wa jangwa, maana yake ni miaka saba ya njaa.
Wakati wa mavuno, sehemu moja ya tano mutamupa mufalme. Sehemu ine zitakazobaki zitakuwa mbegu na chakula kwa ajili yenu na jamaa zenu na watoto wenu.”
Kama vile mvua na teluji inavyoshuka toka mbinguni, wala hairudi kule lakini inalowanisha udongo, kuuzalisha na kuchipukiza mimea, na kumupatia mupandaji mbegu na kuwapa watu chakula,
“Basi ni nani anayekuwa mutumishi mwaminifu na mwenye akili? Ni yule bwana wake aliyemuweka kuwa musimamizi wa watumishi wake wengine na kumwamuru kuwapatia posho yao kwa wakati uliopangwa.
Mungu ndiye anayemupatia mupandaji mbegu na mukate wa kukula. Kwa hiyo atawapatia ninyi mbegu yoyote munayohitaji na kuiotesha, kusudi moyo wenu wa kutoa upate kuzaa matunda mengi.