Mufalme akamupa Yosefu jina la Kimisri: Safenati-Panea. Akamupa Asenati, binti ya Potifera, kuhani wa muji wa Oni kuwa muke wake. Basi, Yosefu akaanza kutembelea inchi nzima ya Misri.
Kisha Yosefu akawaambia watu: “Muangalie, nimekwisha kuwanunua ninyi wote na mashamba yenu kuwa mali ya mufalme. Mutapewa mbegu nanyi mutapanda mashamba yenu.
Ndivyo Yosefu alivyotangaza sheria moja ambayo iko mpaka leo katika inchi ya Misri. Kila mwanainchi anapaswa kutoa sehemu moja ya tano ya mavuno yake kwa mufalme. Udongo wa makuhani tu ndio haukununuliwa na kufanywa mali ya mufalme.
Tunawafahamisha tena kwamba inakatazwa kuwadai kodi ya mapato, malipo ya kuvuka mupaka na mengine makuhani, Walawi, waimbaji, walinzi wa mulango, wafanyakazi au watumishi wengine wa nyumba hii ya Mungu.
Tena nikagundua kwamba Walawi hawakupewa haki zao; na matokeo yake ni kwamba Walawi na waimbaji waliokuwa wakifanya kazi pale mbele, sasa walikwisha kurudilia mashamba yao.
Munajua hakika kuwa wale wanaotumika katika hekalu wanapata chakula chao ndani ya hekalu. Na wale wanaotumika kwa kutoa sadaka juu ya mazabahu wanapata sehemu yao kutoka sadaka zile.
Wazee wa kanisa wanaoongoza kazi yao vizuri wanastahili kupokea mushahara mara mbili, hasa zaidi wale wanaojitolea kwa kufanya kazi ya kuhubiri na kufundisha.