Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 47:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Halafu wakamuletea Yosefu nyama wao: farasi, ngombe, kondoo, mbuzi na punda, naye akawapa chakula. Mwaka ule Yosefu akakuwa anawapa chakula kwa kubadilishana na nyama wao wote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 47:17
7 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yosefu akawaambia: “Kama feza yenu imekwisha, basi munipe nyama wenu, nami nitawapa ngano.”


Mwaka uliofuata wakamufikia tena na kumwambia: “Bwana, ukweli ni kwamba feza yetu yote imekwisha na nyama wetu wamekuwa mali yako. Sasa, bwana, sisi watumishi wako hatuna chochote tunachoweza kukupa isipokuwa miili yetu na mashamba yetu.


Solomono aliagiza farasi kutoka Misri, na vilevile kutoka Kilikia ambako wachuuzi wake waliwanunua.


Shetani akamujibu Yawe: “Ngozi kwa ngozi! Mutu anatoa kila kitu anachokuwa nacho kusudi aokoe maisha yake.


nitanyoosha mukono wangu na kuleta ugonjwa mukali sana juu ya nyama wenu wote: ngombe, farasi, punda, ngamia, mbuzi na kondoo.


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


“Hakuna mutu anayeweza kuwatumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ