Nyuma ya watu wote wa inchi ya Misri na Kanana kutumia feza yao yote, Wamisri wote walimufikia Yosefu na kumwambia: “Utupatie chakula! Kwa nini tukufe mbele ya macho yako? Angalia, sasa feza yetu imekwisha!”
Halafu wakamuletea Yosefu nyama wao: farasi, ngombe, kondoo, mbuzi na punda, naye akawapa chakula. Mwaka ule Yosefu akakuwa anawapa chakula kwa kubadilishana na nyama wao wote.
Kwa kumaliza, wandugu zangu, muweke mafikiri yenu juu ya mambo yote yanayokuwa ya kweli, ya heshima, ya haki, safi, ya kupendeza, nayo mambo yote yanayostahili sifa na ya utu wema.