Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 47:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Yosefu akakuwa anawapatia baba yake, wandugu zake na jamaa yote ya baba yake chakula kulingana na hesabu ya watu waliowategemea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 47:12
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Utakaa karibu nami katika eneo la Goseni: wewe, wana wako na wajukuu wako, nyama wako wa kufugwa na mali yako yote.


Utakapokuwa Goseni, mimi nitakutunza wewe na jamaa yako pamoja na nyama wako kusudi musikufe na njaa, maana kungali miaka mitano zaidi ya njaa.’ ”


Mungu alinileta huku niwatangulie ninyi, kwa kuokoa maisha yenu mubaki wazima katika inchi na kuwakomboa kwa ukombozi mukubwa.


Basi, Yosefu akakwenda kwa mufalme wa Misri, akamwambia: “Baba yangu na wandugu zangu pamoja na kondoo, ngombe na mali yao yote, wamefika kutoka inchi ya Kanana. Sasa wako katika eneo la Goseni.”


na Yosefu akawafanya watu kuwa watumwa, kutoka pembe moja mpaka pembe ingine ya inchi ya Misri.


Wakati wa mavuno, sehemu moja ya tano mutamupa mufalme. Sehemu ine zitakazobaki zitakuwa mbegu na chakula kwa ajili yenu na jamaa zenu na watoto wenu.”


Basi, musiogope. Mimi nitawapa chakula pamoja na watoto wenu.” Basi akawafariji na kusema nao vizuri.


Uwaheshimu baba yako na mama yako, kusudi uishi maisha marefu katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Watu wote na jamaa yake, wadogo kwa wakubwa watajitegemeza kwake kama chungu na vikombe vilivyotundikwa kwenye musumari.


ijapokuwa sisi ni mitume wa Kristo, tungeweza kudai mambo fulani kwenu. Lakini sisi tulionyesha upole kati yenu kama vile mama anavyosumbuka kwa ajili ya watoto wake.


Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.


Lakini kama mujane akiwa na watoto au wajukuu, inafaa wajifunze kwanza kutimiza mapaswa yao ya kidini kwa ajili ya jamaa zao wenyewe na kuwarudishia wazazi na babu zao mema waliyowatendea, kwa maana jambo hilo linamupendeza Mungu.


Kama mutu asipotunza wandugu zake na hasa zaidi watu wa jamaa yake mwenyewe, huyu amekana imani yake naye ni mubaya kuliko mupagani.


Yeye atakurudishia uzima wako na atakutunza katika uzee wako. Mukwe wako ni wa lazima zaidi kwako kuliko watoto wa kiume saba, maana anakupenda na amekuzalia mujukuu huyu!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ