Yawe akamwambia Abramu: “Ujue hakika kwamba wazao wako watakaa kama wageni katika inchi isiyokuwa yao, watakuwa watumwa na watateswa kwa muda wa miaka mia ine.
Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.
Tena Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Nguvu. Ujaliwe wazao wengi na kuongezeka. Taifa na kundi la mataifa watatokea kwako na wafalme watatokea katika uzao wako.
na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote, awabariki vijana hawa! Jina langu na majina ya babu zangu, Abrahamu na Isaka, yadumishwe katika vijana hawa; nao waongezeke kwa wingi katika dunia.”
Lakini baba yake akakataa, akisema: “Ninajua, mwana wangu, ninajua. Wana wa Manase vilevile watakuwa taifa na wakubwa. Hata hivyo, ndugu yake mudogo atakuwa mukubwa kuliko yeye na wazao wake watakuwa mataifa mengi.”
Gedalia aliapa mbele yao na mbele ya waaskari wao akisema: Musiogope kuwatumikia Wakaldea. Mukae katika inchi mumutumikie mufalme wa Babeli, na mambo yote yatawaendekea vema.
na kuniambia: ‘Paulo, usiogope! Sherti usambe mbele ya Mufalme wa Roma. Na tena kwa kuwa inamupendeza Mungu kukutendea mema, yeye ataokoa maisha ya watu hawa wote wanaosafiri pamoja nawe.’
utasema maneno haya mbele ya Yawe, Mungu wako: ‘Baba yangu alikuwa Musuria aliyetangatanga huko na huko, kisha akashuka kwenda Misri akaishi huko kama mugeni. Yeye na jamaa yake walikuwa watu wachache tu walipokuwa huko, lakini wakakuwa taifa kubwa lenye nguvu na watu wengi.