Wachuuzi Wamidiani walipofika pahali pale, wale wandugu wakamwondoa Yosefu katika shimo, wakamwuzisha kwa Waisimaeli kwa bei ya vikoroti makumi mbili vya feza; nao wakamupeleka Yosefu Misri.
Abusaloma pamoja na watu wote wa Israeli wakasema: “Shauri la Husayi ni bora kuliko shauri la Ahitofeli.” Wakakataa shauri la Ahitofeli kwa sababu Yawe alikuwa amepanga kulishinda shauri jema la Ahitofeli kusudi aweze kumuletea Abusaloma hasara.
Ukikaa kimya wakati kama huu, musaada utawafikia Wayuda kutoka pahali pengine, nao wataokolewa; lakini wewe utakufa, na jamaa ya baba yako itaangamia. Ni nani anayejua pengine umefanywa kuwa malkia kwa ajili ya wakati kama huu!”
Kesho yake asubui, Elekana na jamaa yake waliamuka asubui mapema, na kisha kumwabudu Yawe, walirudi kwao Rama. Elekana akalala na muke wake Hana na Yawe akamukumbuka.