Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 45:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Lakini, walipomwelezea yote waliagizwa na Yosefu na alipoona magari aliyopelekewa na Yosefu kwa kumubeba, moyo wake ukajaa furaha kupita kiasi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 45:27
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Uwaambie vilevile wapeleke kutoka hapa magari ya kukokotwa ya kuwaleta watoto wao wachanga na wake zao. Wala wasikose kumuleta baba yao.


Israeli akasema: “Sasa inatosha! Mwana wangu Yosefu yuko muzima! Nitakwenda nimwone mbele ya kufa kwangu.”


Utatukasirikia hata milele? Utadumisha kasirani yako kwa vizazi vyote?


Kama vile maji baridi kwa mwenye kiu, ndivyo habari njema kutoka mbali inavyokuwa.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Nyuma ya siku mbili atatupatia tena uzima. Nyuma ya siku tatu atatufufua kusudi tuweze kuishi pamoja naye.


Mungu akafungua pahali palipokuwa shimo kule Lehi, akatiririsha maji. Samusoni akakunywa maji hayo na nguvu zake zikamurudilia. Chemichemi hiyo ikaitwa “Kisima cha Yule Anayeita” nayo iko kule Lehi mpaka leo.


Vilevile walimupa kipande cha mukate wa tini na vishada viwili vya zabibu zenye kukauka. Alipomaliza kula, akapata nguvu, maana alikuwa hajakula wala kunywa kitu chochote kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ