Basi, Yakobo akaondoka Beri-Seba. Wana wake wakamupeleka yeye, watoto wao wachanga pamoja na wake zao katika magari ambayo mufalme wa Misri alituma kwa kumubeba.
Hivyo basi, kazi yote ya Yawe ikatayarishwa siku hiyo, kwa kufanya Pasaka na kutoa sadaka za kuteketeza kwenye mazabahu ya Yawe; kama vile mufalme Yosia alivyoamuru.
Alitoa sadaka zile kadiri ilivyotakiwa na amri ya Musa kila siku takatifu, ni kusema siku za Sabato, sikukuu za mwandamo wa mwezi, na sikukuu tatu za kila mwaka – sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, sikukuu ya majuma na sikukuu ya vibanda.
Kutoka jangwa la Sini, Waisraeli wote pamoja wakasafiri hatua kwa hatua kama vile Yawe alivyoamuru. Watu wakapiga kambi kule Refidimu. Lakini kule hakukukuwa maji ya kunywa.
Lakini Yawe amefanya sawa kwa maana nimeliasi neno lake. Munisikilize enyi watu wote, muyaangalie mateso yangu. Wabinti zangu na vijana wangu wanaume wamepelekwa katika utumwa.
Watakuja kutoka upande wa kaskazini, pamoja na magari ya vita na ya mizigo, wakiongoza kundi kubwa la watu. Watakuzunguka pande zote kwa ngao kubwa na ndogo na kofia za chuma. Nimewapa uwezo wa kukuhukumu, nao watakuhukumu kadiri ya sheria zao.