Inchi yote ya Misri iko chini yako; uwape baba yako na wandugu zako sehemu bora ya inchi hii. Uwaache wakae katika eneo la Goseni. Na ikiwa unawafahamu watu mashujaa kati yao, uwachague wakuwe waangalizi wa nyama wangu.”
Kwa hiyo, musiwaoeshe na wabinti zenu kwa watu hao, wala musiwaruhusu wana wenu kuwaoa wabinti zao. Pia, musishugulikie usalama au mafanikio yao, kusudi ninyi wenyewe mupate kuwa na nguvu, na mufaidie mema ya inchi hiyo na kuwaachia watoto wenu kama vile urizi milele.’
Sitawaachilia wala sitawaonea huruma. Nitawaazibu kulingana na mienendo yenu, nayo machukizo yenu yangali bado kati yenu. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.
Sitawaachilia wala sitawaonea huruma. Nitawaazibu kulingana na mienendo yenu nayo machukizo yangali bado kati yenu. Halafu mutatambua kwamba ni mimi Yawe ninayewaangamiza.
“Siku ile, yule atakayekutiwa juu ya paa la nyumba, asishuke ndani yake kwa kukamata vitu vyake. Vilevile yule atakayekutiwa katika shamba, asirudie kwake.
Muangamize taifa lolote ambalo Yawe, Mungu wenu atalitia katika mikono yenu, wala musilionee huruma. Musiabudu miungu yao, maana jambo hili litakuwa mutego kwenu.
Waisraeli wametenda zambi, maana wamelivunja agano langu nililowaamuru washike. Wametwaa vimoja kati ya vitu vilivyotolewa viangamizwe. Wameviiba na kudanganya, wakaviweka pamoja na vitu vyao.
Kwa hiyo Daudi akawaambia watu wake: “Kila mutu apakatie upanga wake kwenye kiuno.” Kila mutu akapakatia upanga wake, na Daudi vilevile akapakatia upanga wake. Watu yapata mia ine wakamufuata Daudi na watu mia mbili wakabaki na mizigo.
Hakuna mutu atakayekubaliana na mawazo yenu! Yule aliyekwenda katika vita na yule aliyebaki na mizigo yetu, kila mutu atapewa sehemu inayolingana na ya mwenzake.”