Kisha Yosefu akasema: “Ninyi wenyewe mumeona kwa macho yenu na hata ndugu yangu Benjamina ameona kwa macho yake kwamba ni mimi mwenyewe Yosefu ninayezungumuza nanyi.
Inchi yote ya Misri iko chini yako; uwape baba yako na wandugu zako sehemu bora ya inchi hii. Uwaache wakae katika eneo la Goseni. Na ikiwa unawafahamu watu mashujaa kati yao, uwachague wakuwe waangalizi wa nyama wangu.”
Mordekayi, Muyuda, alikuwa wa kwanza chini ya mufalme Ahasuero katika madaraka. Alipendwa na kuheshimiwa na Wayuda, maana alitumika kwa faida na amani ya watu wake na wazao wao wote.
Lakini kama mujane akiwa na watoto au wajukuu, inafaa wajifunze kwanza kutimiza mapaswa yao ya kidini kwa ajili ya jamaa zao wenyewe na kuwarudishia wazazi na babu zao mema waliyowatendea, kwa maana jambo hilo linamupendeza Mungu.