Mwanzo 45:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Halafu Yosefu akashindwa kujizuia mbele ya wote waliokuwa pamoja naye, akawaamuru watoke inje. Hivyo Yosefu alikuwa peke yake alipojitambulisha kwa wandugu zake.
Mikate hiyo ilipokuwa tayari, Tamari akaiopoa kutoka kikaango. Akamupelekea Amunoni, lakini Amunoni alikataa kula, akaamuru kwamba watu wote watoke inje, na wote wakaondoka.
Yawe anasema hivi: Kwa muda murefu sasa nimenyamaza, nimekaa kimya na kujizuiza; lakini sasa nitalia kama mwanamuke wakati wa kuzaa, anayeugua pamoja na kupumua kwa nguvu.
Lakini ninaposema “Sitamutaja tena Yawe, wala sitasema tena kwa jina lake”, ndani yangu kunawaka kitu kama moto uliofungiwa ndani ya mifupa yangu. Ninajaribu sana kuuzuia humo, lakini ninashindwa.
Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.