Lakini ukipata mumoja kati yetu na sanamu za miungu yako, atakufa! Mbele ya hawa wandugu zetu, onyesha chochote kinachokuwa chako, ukitwae.” Yakobo hakujua kwamba Rakeli alikuwa ameiba sanamu za miungu ya Labani.
Walipoona wamepelekwa kwenye nyumba ya Yosefu, wakashikwa na hofu, wakasema wao kwa wao: “Tumeletwa huku kwa sababu ya ile feza tuliyorudishiwa katika mifuko yetu tulipokuja safari ya kwanza kusudi apate kisingizio cha kutushambulia kwa rafla na kutunyanganya punda wetu na kutufanya watumwa wake.”
Huyo musimamizi akasema: “Sawa. Ikuwe kama mulivyosema. Yeyote atakayepatikana na kikombe hicho, atakuwa mutumwa wangu, lakini wengine wote hamutakuwa na kosa.”
Yuda akamujibu: “Tukuambie nini bwana? Tuseme nini kwa kuonyesha kwamba hatuna kosa? Mungu ameyafichua makosa yetu, sisi watumishi wako. Sasa sisi wote tuko watumwa wako, sisi pamoja na yule aliyepatikana na kikombe chako.”
Kama mimi ni mukosaji au nimefanya kitendo kinachonipasa kuuawa, mimi sikatai kufa. Lakini kama hakuna ukweli wowote katika mashitaki yao juu yangu, hakuna mutu anayeweza kunitoa kwao. Ninaomba kusambishwa na Mufalme wa Roma.”