Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 43:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Mimi mwenyewe nitakuwa rehani kwake. Wewe utanidai mimi. Nisipomurudisha umwone kwa macho yako mwenyewe, kosa likuwe juu yangu milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 43:9
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mimi sikukuletea nyama wako aliyeuawa na nyama wa pori, lakini nilibeba hasara hiyo mimi mwenyewe. Wewe ulinidai nyama aliyeibwa muchana au usiku!


Hapo Rubeni akamwambia baba yake: “Nisipomurudisha Benjamina, uwaue wana wangu wawili. Muache Benjamina katika mikono yangu, nami nitamulinda na kumurudisha kwako.”


Kama tusingalikawia, tungalikuwa tumekwisha kwenda na kurudi mara mbili.”


Damu ya uzima wenu nitaidai. Nitaidai kutoka kwa kila nyama na mwanadamu. Atakayemwua mwanadamu mwenzake, nitamudai uzima wake.


Yule mwanamuke kutoka Tekoa akasema: “Bwana wangu mufalme, makosa yote yakuwe juu yangu na juu ya jamaa ya baba yangu. Hivyo, wewe na ufalme wako musikuwe na kosa.”


Na kama sivyo, itatokea kwamba, wakati wewe bwana wangu mufalme utakapokufa, mimi pamoja na mwana wangu Solomono tutahesabiwa kama wenye kosa.”


Ee Mungu, ujitoe mwenyewe kuwa rehani kwa ajili yangu maana hakuna mwingine wa kujitoa kwa ajili yangu.


Uhakikishe kunisaidia mimi mutumishi wako; usikubali wenye kiburi wanitese.


Nikimwambia mutu mwovu kwamba hakika atakufa, nawe haumwonyi au kumwambia aache mwenendo wake mubaya apate kuyaokoa maisha yake, basi, mutu huyo mwovu atakufa kwa uovu wake; lakini wewe utabeba lazima ya damu yake.


Tena, kama mutu wa haki akigeuka katika haki yake na kutenda uovu, nami nikimwekea kikwazo, mutu huyo atakufa. Kwa vile haukumwonya, atakufa kwa sababu ya zambi yake, nayo matendo yake ya haki hayatakumbukwa. Lakini wewe utabeba lazima ya damu yake.


Lakini kama yule mulinzi akiona waadui wanakuja naye hapigi baragumu na watu wakikosa kuonywa juu ya hatari inayokuja, waadui wakikuja na kumwua mutu yeyote kati yao, huyo mutu aliyekufa, atakuwa amekufa kwa kosa lake. Lakini mimi nitamulaumu mulinzi kwa kifo cha mutu huyo.


Nikimwambia mutu mwovu hivi: Wewe mutu mwovu hakika utakufa; lakini wewe hausemi chochote kwa kumwonya aachane na mwenendo wake, yule mutu atakufa kwa kosa lake; lakini nitakulaumu wewe kwa kifo chake.


Basi watu wa kizazi hiki watabeba lazima ya damu ya manabii wote iliyomwangwa tangu kuumbwa kwa dunia,


Kwa sababu ya kiapo hiki, Yesu amekuwa kihakikisho kwetu cha agano linalokuwa zuri zaidi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ