Mwanzo 43:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
8 Yuda akamwambia baba yake Israeli: “Uniruhusu mimi niende naye kusudi tuondoke mara moja, tuende tununue chakula, tusikufe na njaa pamoja nawe na watoto wetu.
Lakini baba yake akamujibu: “Mwana wangu hatakwenda nanyi. Ndugu yake amekwisha kufa, naye peke yake ndiye aliyebaki. Mimi ni muzee mwenye imvi. Ikiwa kijana huyu atapatwa na hasara yoyote katika safari mutakayofanya basi, mutaniua kwa huzuni.”
nasi tukakuelezea kwamba tuko na baba, naye ni muzee, na kwamba tuko na ndugu mwingine mudogo aliyezaliwa wakati wa uzee wa baba yetu. Kaka yake na yule kijana amekwisha kufa, na yule mudogo ndiye peke yake aliyebaki wa mama yake; na muzee wetu anamupenda sana kijana yule.
tukamwambia: ‘Hatuwezi kwenda, isipokuwa tu kama ndugu yetu mudogo atakwenda pamoja nasi. Kama hatakwenda pamoja nasi hatuwezi kupokelewa na yule mutu.’
Vilevile, Yosefu alisindikizwa na jamaa yake yote, wandugu zake na jamaa yote ya baba yake Yakobo. Katika eneo la Goseni kulibaki watoto wao tu pamoja na kondoo, mbuzi na ngombe wao.
Mumoja kati ya wakubwa wake akasema: “Tafazali, utume watu wachache na farasi watano wa wale waliobaki kusudi waende kuona kumetokea nini. Matokeo yao hayatakuwa mabaya zaidi kuliko Waisraeli wote wanaoangamia hapa.”
Hakuna maana ya kuingia katika muji kwa sababu kule tutakufa. Kwa hiyo kumbe tuende kwenye kambi ya Waaramu. Kama wakituacha kuishi, tutaishi; kama wakituua, tutakufa tu.”
Kisha, nikatoa maagizo kuwa sisi wote tufike karibu na muto Ahara kusudi tufunge kula chakula na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wetu na kumwomba atulinde na kutuongoza katika safari yetu pamoja na watoto wetu.
Ninyi mulisema kwamba watoto wenu watakamatwa mateka, lakini mimi nitawafikisha watoto wenu katika inchi muliyoizarau, kusudi waijue na ikuwe makao yao.