Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 43:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Walipoona wamepelekwa kwenye nyumba ya Yosefu, wakashikwa na hofu, wakasema wao kwa wao: “Tumeletwa huku kwa sababu ya ile feza tuliyorudishiwa katika mifuko yetu tulipokuja safari ya kwanza kusudi apate kisingizio cha kutushambulia kwa rafla na kutunyanganya punda wetu na kutufanya watumwa wake.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 43:18
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha wakasemezana wao kwa wao: “Kweli sisi tulimukosea ndugu yetu. Ingawa tulimwona katika taabu, hatukumujali hata alipotusihi. Ndiyo maana taabu hii yote inatupata.”


Ikakuwa walipofika pahali pa kulala wageni kwa njia, mumoja wao akafungua mufuko wake kusudi apate kumukulisha punda wake, akashangaa kukuta feza yake kwenye kinywa cha mufuko wake.


Akawaambia wandugu zake: “Feza yangu imerudishwa. Ndio hii hapa kwenye kinywa cha mufuko wangu!” Waliposikia hayo, wakavunjika moyo. Wakaangalia wakiwa wanatetemeka na kuulizana: “Ni jambo gani hili Mungu alilotutendea?”


Walipokuwa wanamimina ngano kutoka mifuko yao, wakashangaa kuona kila mumoja wao amerudishiwa kifuko chake na feza ndani ya mufuko wake. Walipoona hayo, wote pamoja na baba yao, wakashikwa na hofu.


Musimamizi yule akafanya kama vile alivyoagizwa. Akawapeleka wale wageni kwenye nyumba ya Yosefu.


Kwa hiyo wakamwendea yule musimamizi wa nyumba ya Yosefu wakaongea naye wakiwa kwa mulango,


Kumbuka, bwana, feza tuliyokuta katika kinywa cha mifuko yetu tuliirudisha kutoka katika inchi ya Kanana. Itawezekana namna gani tena tuibe feza au zahabu kutoka nyumba ya bwana wako?


Sauti za vitisho zitamupigia kelele katika masikio. Anapozani amestawi, mwangamizi atamushambulia.


Wanakuja kama kwenye njia kubwa, na kisha mashambulio wanasonga mbele.


Hao wanaotenda maovu hawajui kitu? Wanatafuna watu wangu kama mikate; wala hawajali Mungu.


Basi, nilijaribu kufikiri juu ya jambo hili, lakini lilikuwa gumu sana kwangu,


Mufalme wa Yuda alipopata habari kwamba Waaramu wanashirikiana na Waisraeli, yeye pamoja na watu wote wa Yuda waliogopa na kutetemeka kama miti inayotikiswa na upepo.


Danieli akaonekana kuwa bora kuliko wale wasimamizi wengine na wakubwa wote kwa maana alikuwa na roho njema. Hivyo mufalme akakusudia kumupa uongozi wa ufalme wote.


Lakini Herode aliposikia habari zile, akasema: “Ni yule Yoane Mubatizaji niliyemukata kichwa ndiye amefufuka!”


Kutokana na amri, zambi ilipata njia hata kuamusha kila namna ya tamaa ndani yangu. Kwa maana pasipo Sheria zambi ingekuwa kama mufu.


na kumushitaki kwamba ametenda mambo ya haya, na kumuharibishia sifa yake kwa kusema kwamba hakukuwa bikira wakati alipomwoa,


na ajabu ni kwamba ameshitaki mambo ya haya na kusema kwamba hakumukuta na ushuhuda wowote kwamba alikuwa bikira. Hata hivyo ushuhuda wa ubikira wa binti yetu ni huu’. Halafu atakunjua nguo yenye huo ushuhuda mbele ya wazee wa muji.


Basi, Manoa akamwambia muke wake: “Hakika tutakufa, maana tumemwona Mungu.”


Wazazi wake hawakujua kwamba ule ulikuwa mupango wa Yawe ambaye alikuwa anatafuta njia ya kushambulia Wafilistini. Wakati ule, Wafilistini walikuwa wakiwatawala Waisraeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ