Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 43:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mungu Mwenye Nguvu awajalie kupata huruma mbele ya mutu yule, awaachie yule ndugu yenu mwingine na Benjamina warudi pamoja nanyi. Kwa upande wangu, ikinipasa kupotelewa na wana wangu, basi!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 43:14
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Kwenda uwakusanye pamoja Wayuda wote wanaokuwa katika muji wa Susani. Mufunge, musikule wala musikunywe kwa siku tatu, usiku na muchana, kwa ajili yangu. Na mimi na wajakazi wangu tutafanya vile vile. Kisha, nitamwendea mufalme, ingawa ni kinyume cha sheria. Kama ni kuuawa, niuawe.”


Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.


Tulipoona kwamba amekataa shauri letu, tukanyamaza na kusema: “Mapenzi ya Bwana yafanyike.”


Ee Bwana, usikilize maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watumishi wako wanaofurahia kukutii wewe. Ninakuomba unifanikishe leo, mimi mutumishi wako, na kunijalia kuhurumiwa na mufalme.” Mimi nilikuwa na madaraka ya kumupa mufalme kinywaji.


Yawe akipendezwa na mwenendo wa mutu, anawageuza hata waadui zake kuwa warafiki.


Wema wako unifikie, ee Yawe; uniokoe kama ulivyoahidi.


Yawe ni muzuri! Wema wake unadumu milele, na uaminifu wake kwa vizazi vyote.


Kwa hiyo, Abrahamu akapaita pahali pale: “Yawe anajalia,” kama inavyosemwa hata leo: “Kwa mulima wa Yawe, watu wanajaliwa.”


Mungu Baba pamoja na Yesu Kristo, Mwana wa Baba, watatujalia neema, huruma na amani katika ukweli na upendo.


Ninakutumia barua hii, wewe Tito, mwana wangu wa kweli katika imani tunayoshiriki pamoja. Ninakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Mwokozi wetu.


lakini kwa sababu hiyo Mungu amenihurumia. Alifanya vile kusudi kwa njia yangu mimi ninayekuwa mutenda zambi wa kwanza, Yesu Kristo apate kuonyesha uvumilivu wake. Na hivi mimi nipate kuwa mufano kwa wote watakaoamini nyuma na kupata uzima wa milele.


Ninakuandikia wewe Timoteo mwana wangu wa kweli katika imani. Ninakutakia neema na rehema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.


akamwokoa toka katika taabu yote aliyopata. Mungu akamujalia neema, apate kupendwa na Mufalme wa Misri na kuonekana kuwa mwenye hekima mbele yake. Mufalme yule akamuweka kuwa musimamizi wa inchi yake na wa nyumba yake yote.


Yeye anawasikilia wale wanaomwogopa huruma kwa vizazi vyote.


Muimbe kwa furaha, enyi mbingu! Ushangilie ewe dunia, Enyi milima, mulalamike kwa furaha, maana Yawe amewafariji watu wake, anawaonea huruma watu wake wanaoteseka.


Moyo wa mufalme ni kama maji yanayotiririka; Yawe anauongoza popote anapopenda.


Hizi ni mezali za Solomono mwana wa Daudi mufalme wa Israeli.


Ezra akasema: “Asifiwe Yawe, Mungu wa babu zetu, ambaye amemupatia mufalme moyo wa kupamba nyumba ya Yawe inayokuwa Yerusalema.


Baba yao Yakobo, akawaambia: “Munaniondolea watoto wangu! Yosefu hayuko, Simeoni hayuko, sasa munataka kumutwaa Benjamina. Hayo yote yanaanguka juu yangu!”


Yosefu akakwenda pembeni, akaanza kulia. Alipotulia, akarudi kuzungumuza nao. Kisha akamukamata Simeoni na kumufunga mbele ya macho yao.


Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kumutendea mema, hata kumufanya apate kukubaliwa mbele ya mukubwa wa kifungo.


Tena Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Nguvu. Ujaliwe wazao wengi na kuongezeka. Taifa na kundi la mataifa watatokea kwako na wafalme watatokea katika uzao wako.


Mungu Mwenye Nguvu akubariki upate wazao wengi na kuongezeka, kusudi ukuwe jamii kubwa ya watu.


Hautatujalia tena maisha mapya, kusudi watu wako wafurahi kwa sababu yako?


Pilato akajibu: “Yale niliyoandika, yameandikwa!”


Mumupeleke vilevile ndugu yenu muende kwa yule mutu.


Aliwafanya wale waliowaangamiza wawaonee huruma.


Yule musimamizi akapekua mifuko yote, akianza na wakubwa wao na kumalizia na mudogo kabisa. Kikombe kikapatikana katika mufuko wa Benjamina.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ