Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 43:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Mupeleke feza mara mbili ya ile inayohitajika, kwa sababu ni lazima murudishe feza ile iliyowekwa kwenye kinywa cha mifuko yenu; pengine ilirudishwa kwa makosa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 43:12
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yosefu akatoa amri wajaze mifuko yao na ngano na kumurudishia kila mumoja feza yake katika mufuko wake, na kuwapa chakula cha njia. Wakafanyiwa mambo hayo yote.


Walipokuwa wanamimina ngano kutoka mifuko yao, wakashangaa kuona kila mumoja wao amerudishiwa kifuko chake na feza ndani ya mufuko wake. Walipoona hayo, wote pamoja na baba yao, wakashikwa na hofu.


Mumupeleke vilevile ndugu yenu muende kwa yule mutu.


Tulipofika pahali pa kulala wageni kule katika njia, tukafungua mifuko yetu, tukashangaa kukuta feza ya kila mumoja wetu kwenye kinywa cha mufuko wake bila kuguswa. Sasa tumerudisha feza hiyo.


Tumeleta na feza ingine kwa kununua chakula. Hatujui ni nani aliyeweka feza yetu katika mifuko yetu.”


Musimurudishie mutu ubaya kwa ubaya. Mukuwe na roho ya kufanya mema mbele ya watu wote.


Musikuwe na deni la mutu yeyote. Deni moja munalopaswa kuwa nalo ni kupendana. Kwa maana yule anayemupenda mwenzake ametimiza Sheria kabisa.


Kwa maana tunataka kufanya mema, si mbele ya Bwana tu, lakini mbele ya watu vilevile.


Kwa kumaliza, wandugu zangu, muweke mafikiri yenu juu ya mambo yote yanayokuwa ya kweli, ya heshima, ya haki, safi, ya kupendeza, nayo mambo yote yanayostahili sifa na ya utu wema.


Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.


Lakini muchunguze kila jambo na kushika lile linalokuwa jema.


Yesu Kristo ni yule yule, jana, leo na hata milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ