Mwanzo 43:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Mupeleke feza mara mbili ya ile inayohitajika, kwa sababu ni lazima murudishe feza ile iliyowekwa kwenye kinywa cha mifuko yenu; pengine ilirudishwa kwa makosa.
Yosefu akatoa amri wajaze mifuko yao na ngano na kumurudishia kila mumoja feza yake katika mufuko wake, na kuwapa chakula cha njia. Wakafanyiwa mambo hayo yote.
Walipokuwa wanamimina ngano kutoka mifuko yao, wakashangaa kuona kila mumoja wao amerudishiwa kifuko chake na feza ndani ya mufuko wake. Walipoona hayo, wote pamoja na baba yao, wakashikwa na hofu.
Tulipofika pahali pa kulala wageni kule katika njia, tukafungua mifuko yetu, tukashangaa kukuta feza ya kila mumoja wetu kwenye kinywa cha mufuko wake bila kuguswa. Sasa tumerudisha feza hiyo.
Kwa kumaliza, wandugu zangu, muweke mafikiri yenu juu ya mambo yote yanayokuwa ya kweli, ya heshima, ya haki, safi, ya kupendeza, nayo mambo yote yanayostahili sifa na ya utu wema.
Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.