Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 42:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Wakati ule Yosefu alikuwa mukubwa kule Misri. Yeye ndiye aliyekuwa akiwauzishia wanainchi ngano. Basi, kaka zake wakakuja na kuinama mbele ya Yosefu kwa heshima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 42:6
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alipoinua macho yake, akaona watu watatu wakisimama mbali kidogo mbele yake. Mara tu alipowaona, akakimbia kutoka kwenye mulango wa hema yake, akakwenda kuwapokea. Alipowafikia akainama kwa heshima


Wale wamalaika wawili wakafika katika muji wa Sodoma magaribi. Loti alikuwa ameketi kwenye mulango wa muji wa Sodoma. Alipowaona, akasimama kwenda kuwapokea, akainama kwa heshima.


Kisha yeye mwenyewe akawatangulia. Akakwenda akiinama uso mpaka chini kwa heshima mara saba, mpaka alipofika karibu na ndugu yake.


Mufalme akamupandisha katika gari lake la pili na walinzi wakatangulia mbele ya Yosefu wakilalamika kwa sauti na kusema: “Mupige magoti!” Ndivyo mufalme alivyomupa Yosefu madaraka makubwa juu ya inchi yote ya Misri.


Ikaanza miaka saba ya njaa kama vile Yosefu alivyokuwa amesema pale mbele. Inchi zingine zote zikakuwa na njaa, lakini inchi yote ya Misri ilikuwa na chakula.


Zaidi ya hayo, watu toka kila pahali katika dunia walikuja Misri kwa Yosefu kununua ngano, maana njaa ilikuwa kali katika dunia yote.


Yuda na wandugu zake wakafika kwa Yosefu naye Yosefu alikuwa bado katika nyumba. Basi, wakainama mbele yake kwa heshima,


Wakamwambia baba yao: “Yosefu iko muzima! Yeye ndiye mutawala wa inchi yote ya Misri!” Hapo baba yao akapigwa na bumbuazi, maana hakuweza kuyasadiki maneno yao.


Kwa hiyo, si ninyi mulionileta huku, lakini ni Mungu. Ndiye aliyenifanya kama baba kwa mufalme wa Misri, musimamizi wa nyumba yake yote na mutawala wa inchi yote ya Misri.


Hapo Yosefu akawaondoa wana wake kwenye magoti ya baba yake, kisha akainama kwa heshima.


Watu wanamulaani mutu anayeficha ngano, lakini wanamutakia baraka mwenye kuiuzisha.


Wazao wa wale waliokutesa, watakuja na kuinama uso mpaka chini mbele yako. Wote wale waliokuzarau, watapiga magoti kwenye miguu yako. Watakuita: “Muji wa Yawe”, “Sayuni”, “Muji wa Mutakatifu wa Israeli”.


akamwokoa toka katika taabu yote aliyopata. Mungu akamujalia neema, apate kupendwa na Mufalme wa Misri na kuonekana kuwa mwenye hekima mbele yake. Mufalme yule akamuweka kuwa musimamizi wa inchi yake na wa nyumba yake yote.


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


Yule kijana alipokwisha kuondoka, Daudi akasimama na kutoka pahali alipojificha karibu na lundo la mawe. Aliinama chini kwa heshima mara tatu mbele ya Yonatani. Wote wawili, Daudi na Yonatani, wakakumbatiana na kulia. Daudi alikuwa na uchungu zaidi kuliko Yonatani.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ