Mutume mumoja wenu amulete yule ndugu yenu mudogo, wakati wengine wenu wanamungoja katika kifungo. Kwa hiyo ukweli wa maneno yenu utajulikana. Kama sivyo, ninaapa kwa jina la mufalme wa Misri kwamba ninyi ni wapelelezi.”
Yosefu alipoona kaka zake akawatambua, lakini akajifanya sawa vile hawafahamu, akasema nao kwa ukali. Akawauliza: “Mumetoka wapi ninyi?” Wakamujibu: “Tumetoka katika inchi ya Kanana, tumekuja kununua chakula.”