Akawaambia wandugu zake: “Feza yangu imerudishwa. Ndio hii hapa kwenye kinywa cha mufuko wangu!” Waliposikia hayo, wakavunjika moyo. Wakaangalia wakiwa wanatetemeka na kuulizana: “Ni jambo gani hili Mungu alilotutendea?”
Wakamwambia baba yao: “Yosefu iko muzima! Yeye ndiye mutawala wa inchi yote ya Misri!” Hapo baba yao akapigwa na bumbuazi, maana hakuweza kuyasadiki maneno yao.