Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 42:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Yosefu akakwenda pembeni, akaanza kulia. Alipotulia, akarudi kuzungumuza nao. Kisha akamukamata Simeoni na kumufunga mbele ya macho yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 42:24
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha siku tatu, waliotahiriwa wakiwa wangali na maumivu makali, wana wawili wa Yakobo, Simeoni na Lawi, kaka za Dina, wakatwaa panga zao, wakashambulia muji kwa rafla na kuwaua wanaume wote.


Wao hawakujua kwamba Yosefu alielewa yote yale waliyosema, maana alipoongea nao ilikuwa kwa njia ya mutafsiri.


Mungu Mwenye Nguvu awajalie kupata huruma mbele ya mutu yule, awaachie yule ndugu yenu mwingine na Benjamina warudi pamoja nanyi. Kwa upande wangu, ikinipasa kupotelewa na wana wangu, basi!”


Yule musimamizi akawajibu: “Musikuwe na wasiwasi, wala musiogope. Bila shaka Mungu wenu, Mungu wa baba yenu, ndiye aliyewarudishia feza katika mifuko yenu. Mimi nilipokea feza yenu.” Kisha akawaletea Simeoni, ndugu yao.


Yosefu akatoka pahali pale kwa haraka, kwa sababu ya hamu kubwa juu ya ndugu yake, akatafuta pahali pa kulilia. Akaingia ndani ya chumba chake na kuanza kulia.


Halafu Yosefu akashindwa kujizuia mbele ya wote waliokuwa pamoja naye, akawaamuru watoke inje. Hivyo Yosefu alikuwa peke yake alipojitambulisha kwa wandugu zake.


Lakini akalia kwa sauti kubwa hata Wamisri wakamusikia. Vilevile watu wa jamaa ya mufalme nao wakamusikia.


Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.


Yesu alipokaribia muji wa Yerusalema, na alipouona, akaulilia,


Mufurahi pamoja na wenye kufurahi. Mulie pamoja na wenye kulia.


Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote vinaugua pamoja nacho. Kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vingine vyote vinafurahi pamoja nacho.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ