Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 42:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Kisha mumulete kwangu ndugu yenu mudogo. Hii itahakikisha ukweli wa maneno yenu, nanyi hamutauawa.” Basi, wakakubali kufanya hivyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 42:20
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hivi ndivyo mutakavyojaribiwa: Ninaapa kwa jina la mufalme wa Misri, kwamba hamutatoka hapa mpaka mudogo wenu atakapokuja.


kama kweli ninyi ni watu waaminifu, mumoja wenu abaki katika kifungo na wengine wapeleke ngano kwa jamaa zenu wenye njaa.


Wakabebesha punda wao mizigo yao ya ngano, wakaondoka.


Halafu mukubwa wa inchi hiyo akatuambia: ‘Hivi ndivyo nitakavyotambua kwamba kweli ninyi ni watu waaminifu. Muniachie kwangu ndugu yenu mumoja, nanyi wengine mupeleke ngano kwa jamaa zenu wenye njaa.


Kisha muniletee yule ndugu yenu mudogo, na hapo nitajua kwamba ninyi si wapelelezi lakini ni watu waaminifu. Mukifanya hivyo nitamwacha huru ndugu yenu, nanyi mutaruhusiwa kufanya biashara katika inchi hii.’ ”


Kwa hiyo wakamwendea yule musimamizi wa nyumba ya Yosefu wakaongea naye wakiwa kwa mulango,


Lakini Yuda akamwambia baba yake: “Yule mutu alituonya vikali, akisema: ‘Sitawapokea musipokuja na ndugu yenu mudogo.’


Lakini ikiwa hautakubali aende nasi, basi, hatutakwenda kule, maana yule mutu alituambia waziwazi: ‘Hamutaniona musipokuja na ndugu yenu mudogo.’ ”


Bwana, ulituagiza sisi watumishi wako kumuleta yule mudogo wetu upate kumwona.


Lakini wewe bwana ukatuambia kwamba kama hatutakuja na ndugu yetu mudogo, hautatupokea tena.


Noa akafanya yote kama vile Mungu alivyomwamuru.


Halafu mama yake akawaambia watumishi: “Mufanye kila kitu atakachowaambia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ