Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 42:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Wakamwambia: “Sisi, watumishi wako, tuko wandugu kumi na wawili, wana wa mutu mumoja, mwenyeji wa inchi ya Kanana. Mudogo wetu amebaki na baba kwa nyumba na ndugu yetu mwingine ni marehemu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 42:13
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

akaendea wandugu zake, akawaambia: “Kijana hayuko, nami niende wapi?”


Sisi ni ndugu, wana wa baba mumoja. Sisi ni watu waaminifu, wala si wapelelezi.”


Lakini Yosefu akawaambia: “Sivyo! Mumekuja hapa kwa kupeleleza uzaifu wa inchi yetu.”


Lakini Yosefu akawaambia: “Ni kama vile nilivyosema: ninyi ni wapelelezi tu.


Tukamwelezea kwamba sisi tuko wandugu kumi na wawili wa baba mumoja. Mumoja wetu ni marehemu na yule mudogo yuko kwetu katika inchi ya Kanana pamoja na baba yetu.


Baba yao Yakobo, akawaambia: “Munaniondolea watoto wangu! Yosefu hayuko, Simeoni hayuko, sasa munataka kumutwaa Benjamina. Hayo yote yanaanguka juu yangu!”


Lakini baba yake akamujibu: “Mwana wangu hatakwenda nanyi. Ndugu yake amekwisha kufa, naye peke yake ndiye aliyebaki. Mimi ni muzee mwenye imvi. Ikiwa kijana huyu atapatwa na hasara yoyote katika safari mutakayofanya basi, mutaniua kwa huzuni.”


Yosefu alipoinua macho yake na kumwona Benjamina, ndugu yake, mutoto wa mama yake, akasema: “Huyu ndiye ndugu yenu mudogo muliyeniambia habari zake? Mungu akubariki, mwana wangu!”


Wakamujibu: “Yule mutu alituuliza kwa makali sana juu ya mambo yetu na jamaa yetu akisema: ‘Baba yenu angali muzima? Muko na ndugu mwingine?’ Hivyo tukamujibu kulingana na maulizo yake. Tungaliweza namna gani kujua kwamba atatuambia: ‘Mulete ndugu yenu?’ ”


nasi tukakuelezea kwamba tuko na baba, naye ni muzee, na kwamba tuko na ndugu mwingine mudogo aliyezaliwa wakati wa uzee wa baba yetu. Kaka yake na yule kijana amekwisha kufa, na yule mudogo ndiye peke yake aliyebaki wa mama yake; na muzee wetu anamupenda sana kijana yule.


mumoja alitoweka, nami nikasema, bila shaka ameraruliwa vipandevipande na nyama wa pori, maana sijapata kumwona tena.


Wakamwambia baba yao: “Yosefu iko muzima! Yeye ndiye mutawala wa inchi yote ya Misri!” Hapo baba yao akapigwa na bumbuazi, maana hakuweza kuyasadiki maneno yao.


Yawe anasema hivi: Sauti imesikilika katika muji wa Rama, maombolezo na kilio cha uchungu. Rakeli anawalilia watoto wake, wala hataki kufarijiwa kwa ajili yao, maana wote hawako tena.


Babu zetu walitenda zambi na sasa hawako tena; nasi tunabeba makosa yao.


Herode alipoona kwamba wale watu wenye elimu wamemudanganya, akakasirika sana. Akatuma watu Betelehemu na popote kandokando yake kwa kuua watoto wote waliokuwa na umri wa miaka miwili na chini yake. Alifanya vile kufuatana na jinsi alivyohakikishwa na wale wenye elimu juu ya wakati nyota ilipotokea.


“Sauti inasikilika toka Rama, kilio na malalamiko mengi. Ni Rakeli anayewalilia watoto wake, naye hataki kufarijiwa, kwa maana hawako tena.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ