Mutume mumoja wenu amulete yule ndugu yenu mudogo, wakati wengine wenu wanamungoja katika kifungo. Kwa hiyo ukweli wa maneno yenu utajulikana. Kama sivyo, ninaapa kwa jina la mufalme wa Misri kwamba ninyi ni wapelelezi.”
Wakamujibu: “Yule mutu alituuliza kwa makali sana juu ya mambo yetu na jamaa yetu akisema: ‘Baba yenu angali muzima? Muko na ndugu mwingine?’ Hivyo tukamujibu kulingana na maulizo yake. Tungaliweza namna gani kujua kwamba atatuambia: ‘Mulete ndugu yenu?’ ”
Mutu anayesema kwa mamlaka yake mwenyewe, anajitafutia sifa yake mwenyewe. Lakini yeye anayetafuta sifa ya yule aliyemutuma, huyu ni mwenye ukweli wala hana ubaya wowote.