Ikaanza miaka saba ya njaa kama vile Yosefu alivyokuwa amesema pale mbele. Inchi zingine zote zikakuwa na njaa, lakini inchi yote ya Misri ilikuwa na chakula.
Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kusikia sauti ya baragumu juu ya mulima uliokuwa unafuka moshi, wote wakaogopa na kutetemeka. Wote wakasimama mbali,
Watu wanauliza: Kwa nini sisi tunakaa tu hapa? Tukusanyike, tuingie katika miji yenye kuzungukwa na kuta, tuangamie kule! Yawe, Mungu wetu, amekusudia tuangamie, ametupa maji yenye sumu tukunywe, kwa sababu tumemukosea yeye.
Watu wa Efuraimu walipogundua ugonjwa wao, watu wa Yuda walipogundua kidonda chao, watu wa Efuraimu walikwenda Asuria kuomba musaada kwa mufalme mukubwa; lakini yeye hakuweza kuwatunza, hakuweza kuponyesha kidonda chao.
Lakini walitambua kuwa Mungu amenipatia kazi ya kuhubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine sawa alivyomupatia Petro kazi ya kuihubiri kwa Wayuda.