Lakini uliongolewa kwa hasira, ukatupwa chini juu ya udongo; upepo mukali wa mashariki ukaukausha, matunda yake yakaanguka; matawi yake yenye nguvu yalikauka, nao moto ukauteketeza.
Hata kama Efuraimu atastawi kama nyasi, mimi Yawe nitavumisha upepo mukali wa mashariki, upepo utakaotokea kule katika jangwa, nao utakausha visima vyake, chemichemi zake zitakauka. Vitu vyake vyote vya bei kali vitaharibiwa.
Jua lilipotokea, Mungu akaleta upepo mukali kutoka upande wa jangwa, jua likamuchoma sana Yona juu ya kichwa, karibu azimie. Akatamani kufa, akisema: Ni vizuri kwangu kufa kuliko kuishi.