Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 41:55 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

55 Wakati wanainchi wa Misri walipoanza kuona njaa, wakamulilia mufalme awape chakula. Naye akawaambia Wamisri wote: “Mwende kwa Yosefu; mufanye neno lolote atakalowaambia.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 41:55
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Njaa ikazidi kuwa kali na kuenea katika inchi yote. Kwa hiyo Yosefu akafungua gala zote, akawauzishia Wamisri chakula.


Wakati ule Yosefu alikuwa mukubwa kule Misri. Yeye ndiye aliyekuwa akiwauzishia wanainchi ngano. Basi, kaka zake wakakuja na kuinama mbele ya Yosefu kwa heshima.


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Halafu mama yake akawaambia watumishi: “Mufanye kila kitu atakachowaambia.”


Basi, kwa njia ya Yesu Kristo, Mungu wangu atatimiza mahitaji yenu yote kufuatana na uwingi na utukufu wa utajiri wake.


Kwa maana Mungu mwenyewe alitaka ukamilifu wake uonekane ndani ya mwana wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ