Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 41:52 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

52 Mwana wake wa pili akamwita Efuraimu, akisema: “Mungu amenipa watoto katika inchi ya mateso yangu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 41:52
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitakufanya ukuwe na wazao wengi sana. Toka kwako nitatokeza mataifa mengi na wafalme.


Mungu Mwenye Nguvu akubariki upate wazao wengi na kuongezeka, kusudi ukuwe jamii kubwa ya watu.


Yosefu akamwita mwana wake wa kwanza Manase, akisema: “Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote na jamaa ya baba yangu.”


Miaka ile saba ya shibe katika inchi ya Misri ikapita.


Nyuma ya mambo hayo, Yosefu akapewa habari kwamba baba yake ni mugonjwa. Hivyo, akatwaa wana wake wawili, Manase na Efuraimu, akakwenda nao kwa baba yake.


Lakini Israeli akaipishanisha mikono yake: mukono wake wa kuume akauweka juu ya kichwa cha Efuraimu, ingawa alikuwa mudogo na mukono wake wa kushoto akauweka juu ya kichwa cha Manase, aliyekuwa muzaliwa wa kwanza.


Yakobo akaendelea kusema: “Wana wako wawili uliowapata hapa Misri mbele sijafika, ni wana wangu. Efuraimu na Manase watakuwa wangu kama vile Rubeni na Simeoni wanavyokuwa.


“Yosefu ni kama muti unaozaa, muti unaozaa kando ya chemichemi, matawi yake yanatanda kwenye ukuta.


Yosefu alijaliwa kuwaona watoto na wajukuu wa mwana wake Efuraimu na vilevile kuwapokea kama wana wake watoto wa Makiri mwana wa Manase.


Munakunywa divai katika mabakuli, na kujipakaa marasi mazuri kabisa. Lakini hamuhuzuniki hata kidogo juu ya kuangamia kwa wazao wa Yosefu.


Kabila la Yosefu baba ya Manase na Efuraimu.


akamwokoa toka katika taabu yote aliyopata. Mungu akamujalia neema, apate kupendwa na Mufalme wa Misri na kuonekana kuwa mwenye hekima mbele yake. Mufalme yule akamuweka kuwa musimamizi wa inchi yake na wa nyumba yake yote.


Wazao wa Yosefu walikuwa makabila mawili: Manase na Efuraimu. Kabila la Lawi halikupewa sehemu yoyote ya inchi, lakini miji tu ya kuishi na mashamba ya malisho kwa ajili ya nyama wao na riziki zao.


Wazao wa Yosefu, ni kusema kabila la Manase na kabila la Efuraimu, walipewa inchi hiyo kuwa urizi wao.


Watu wa kabila la Manase ambaye alikuwa muzaliwa wa kwanza wa Yosefu, vilevile walipewa eneo lao kwa kura. Makiri, muzaliwa wa kwanza wa Manase baba ya Gileadi, alikwisha kupewa kwa kura miji ya Gileadi na Basani, maana alikuwa hodari katika vita.


Hivyo Hana akapata mimba, akazaa mutoto wa kiume. Hana akamwita mutoto huyo Samweli, maana alisema: “Nimemwomba kwa Yawe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ