Nyuma ya mambo hayo, Yosefu akapewa habari kwamba baba yake ni mugonjwa. Hivyo, akatwaa wana wake wawili, Manase na Efuraimu, akakwenda nao kwa baba yake.
Yakobo akaendelea kusema: “Wana wako wawili uliowapata hapa Misri mbele sijafika, ni wana wangu. Efuraimu na Manase watakuwa wangu kama vile Rubeni na Simeoni wanavyokuwa.
Basi, mwenye kujitakia baraka katika inchi, atajitakia baraka kwa Mungu wa kweli. Mwenye kuapa katika inchi hii, ataapa kwa Mungu wa kweli. Maana taabu za zamani zimepita zimetoweka kabisa mbele yangu.
Utukufu wake ni utukufu wa ngombe dume wa kwanza, pembe zake ni za mbogo dume. Atazitumia kusukuma mataifa; yote atayasukuma mpaka miisho ya dunia. Efuraimu atakuwa na pembe hizo elfu kumi na Manase kwa maelfu.”
Wazao wa Yosefu walikuwa makabila mawili: Manase na Efuraimu. Kabila la Lawi halikupewa sehemu yoyote ya inchi, lakini miji tu ya kuishi na mashamba ya malisho kwa ajili ya nyama wao na riziki zao.
Watu wa kabila la Manase ambaye alikuwa muzaliwa wa kwanza wa Yosefu, vilevile walipewa eneo lao kwa kura. Makiri, muzaliwa wa kwanza wa Manase baba ya Gileadi, alikwisha kupewa kwa kura miji ya Gileadi na Basani, maana alikuwa hodari katika vita.